• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wanafunzi Watakiwa Kulinda Amani

Posted on: August 14th, 2017

Wanafunzi Watakiwa Kulinda Amani

Wanafunzi wa Shule za Sekondari katika Halmashauri ya Mji Geita wameagizwa kutoa taarifa sahihi juu ya masuala ya rushwa yanayojitokeza katika mazingira yao ili  kulinda Amani iliyopo katika nchi ya Tanzania, kwani endapo watazembea na kuipoteza Amani itawawia vigumu kuitafuta pindi itakapotoweka.

Agizo hilo limetolewa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2017 Ndg. Amour Hamad Amour alipokuwa akigawa zawadi kwa wanafunzi walioongoza nafasi tatu bora katika mashindano ya uandishi wa insha yaliyofanywa na klabu ya kupinga na kuzuia Rushwa katika Shule ya Sekondari Ihanamilo mjini Geita.

Ndg. Amour Hamad Amour amefafanua kuwa tatizo la rushwa limeota mizizi katika jamii yetu na linaleta athari kama wananchi kukosa huduma za afya za uhakika, vifo, kukosekana kwa ajira kwa watu wanaostahili, hivyo ni wajibu wa kila Mtanzania kulingana na nafasi aliyonayo kuhakikisha kuwa anapambana ili kuondokana na   tatizo la rushwa.

Pia amewapongeza wanafunzi watatu kutoka Shule za Sekondari Geita, Sekondari ya wasichana Nyankumbu na Shule ya Sekondari Geita Adventist kwa uhodari na ubunifu mkubwa katika uandishi wa Insha zenye mawazo ya kujenga zilizokuwa na ujumbe “ Tuungane kwa pamoja dhidi ya Rushwa kwa Amani na Usalama wa nchi yetu.”

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa amesifu jitihada za Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa( TAKUKURU) Mkoa wa Geita kwa kazi nzuri wanayoifanya katika kuhakikisha suala la vita juu ya rushwa linatekelezwa. Ameongeza kuwa, tatizo la rushwa lipo katika kila eneo  ambapo shughuli za maendeleo hufanyika hivyo elimu ya kupambana nayo inatakiwa kutolewa Zaidi kwa vijana wa Taifa la leo.

“ Vijana ni lazima wajengewe mazingira mazuri kimaisha ili waweze kujikwamua kimaendeleo. Hivyo natoa wito kwa Wazazi, walimu na viongozi mbalimbali wa Serikali katika ngazi zote kuhakikisha mnawasaidia vijana hao kutimiza ndoto zao. Pia wanafunzi mnatakiwa kuwa na nidhamu kwa walimu wenu, wazazi, walezi na wanafunzi wenzenu ili kuwa na Taifa imara na lenye maendeleo.

Mradi wa klabu ya Kuzuia na kupambana na Rushwa katika Shule ya Sekondari Ihanamilo ni  miongoni mwa  Miradi  iliyozinduliwa na Mbio za Mwenge wa Uhuru Mwaka 2017 katika Halmashauri ya Mji Geita. Ambapo jumla ya Shilingi 1,075,000/-( Milioni moja na elfu na sabini na tano) zimetumika kufanikisha Mradi huo.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa