• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Geita Mji Yang'ara Kwa Utoaji Mikopo

Posted on: August 15th, 2017

Geita Mji Yang’ara kwa Utoaji Mikopo

Halmashauri ya Mji Geita imefanya vizuri kwa kutimiza agizo la Serikali la kutoa asilimia kumi(10%) ya bajeti yake kama Mikopo kwa vikundi vya vijana na kina mama wanaojishughulisha na kazi mbalimbali zinazowakwamua kiuchumi.

Akizungumza wakati wa  utoaji wa Hundi kwa vikundi sita vya vijana na wanawake wajasiriamali kutoka kata mbalimbali za Halmashauri ya Mji Geita wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2017 katika uwanja wa Shule ya Sekondari Kalangalala. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Geita, Mh. Leonard K. Bugomola amesema kuwa Halmashauri ya Mji Geita inatambua na kuthamini shughuli za kiuchumi  zinazofanywa na vijana pia wanawake walio jisajili katik a vikundi, hivyo kwa Mwaka wa fedha 2017/2018 Halmashauri imetenga bajeti ya Shilingi Milioni Mia tano( 500,000,000/-) zitakazokopeshwa kwa vikundi vilivyosajiliwa katika Halmashauri  ya Mji wa Geita.

Hundi tofauti zenye jumla ya Shilingi Milioni thelethini(30,000,000/-) zilitolewa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2017 Ndg. Amour Hamad Amour kwa vikundi sita vya wanawake na vijana waliojiajiri katika shughuli mbalimbali za kiuchumi katika Halmashauri ya Mji wa Geita.

Ndg. Amour ameipongeza Halmashauri ya Mji Geita kwa kutoa fedha inayotosheleza kulingana na agizo lililotolewa na Serikali la kutenga asilimia 10% ya bajeti yake kutoa mikopo kwa vikundi vya wanawake na vijana waliojiajiri.  Aliwataka Wakurugenzi ambao wanakwepa kutoa fedha hizo kiutaratibu waige mfano wa Halmashauri ya Mji Geita.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2017 alitoa pongezi kwa vijana waliojikwamua kwa kujiajiri katika shughuli mbalimbali za maendeleo na kwa kuzalisha. bidhaa zenye viwango na zinazovutia. Kadhalika aliwataka wawe mabalozi wazuri kwa vijana ambao wako mitaani na hawataki kujishughulisha bali hushinda wakicheza bao na kutoa shutuma zisizofaa kwa Serikali.

Pia aliwaagiza wataalam  wa Idara ya Maendeleo ya jamii kuendelea kutoa mafunzo kwa vijana hao na kuwasaidia kuwatafutia vifungashio bora vya bidhaa zao ili kukidhi ushindani wa biashara kitaifa na kimataifa. Ndg. Amour aliwashauri wataalam hao kujifunza juu ya kilimo cha nyumba ya kijani (green house) kwani ni kilimo kilicho katika soko la biashara kimataifa ili wawashawishi vijana katika umoja wao kulima kilimo hiki chenye tija.

Ndg. Amour Hamad Amour alitoa wito kwa Halmashauri ya Mji Geita kuunda SACCOS itakayotumika kupewa fedha zote ambazo wanavikundi walio ndani ya SACCOS watakopeshwa fedha hizo. Hii itasaidia usalama wa fedha inayokopeshwa kuwa wa uhakika zaidi kuliko utaratibu unaotumika hivi sasa wa kukopesha vikundi moja kwa moja.

Ukiwa Halmashauri ya Mji wa Geita, Mwenge wa Uhuru umezindua, kufungua, kuweka mawe ya msingi katika Miradi kumi ambapo miradi minne ilitembelewa. Miradi  yote ina thamani ya Shilingi 9,177,774,739.73 ambapo Halmashauri imechangia Shilingi 259,620,989.73, Serikali kuu imechangia Shilingi 331,692,500 na Shilingi 8,586,461,250 ni nguvu kazi za wananchi.

Ujumbe wa Mwenge wa Uhuru mwaka 2017 ni “SHIRIKI KUKUZA UCHUMI WA VIWANDA KWA MAENDELEO YA NCHI YETU”.




Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa