• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Ziara Za Mafunzo Kuboresha Kiwango Cha Ufaulu

Posted on: May 13th, 2021

Ziara Za Mafunzo Kuboresha Kiwango Cha Ufaulu

Walimu kutoka katika Shule za Msingi na Sekondari ndani ya Halmashauri ya Mji wa Geita ambazo hazikufanya vizuri kitaaluma hususan katika mitihani ya kuhitimu mwaka 2020 na miaka ya nyuma wameshauriwa kufanya ziara za mafunzo kwenye shule ambazo zina ufaulu mzuri.

Ushauri huo umetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita Mheshimiwa Joseph Lugaila ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kikao cha wadau wa elimu waliokutana  kujadili kwa pamoja maendeleo ya sekta ya elimu katika Halmashauri ya Mji wa Geita  kwenye ukumbi wa Shule ya Sekondari ya wasichana Nyankumbu hivi karibuni.

Mhe. Lugaila aliongeza kuwa  ziara za mafunzo katika shule zinazofanya vizuri kitaaluma zitawawezesha walimu wa shule zinazofanya vibaya kujifunza mbinu za kufundisha na masuala mengine muhimu yatakayowawezesha kupandisha kiwango cha ufaulu katika shule zao. Pia wahakikishe wazazi na walezi wa wanafunzi wanashirikishwa katika vikao mbalimbali na mipango yote iliyopangwa kutekelezwa shuleni.

Akiongelea mikakati iliyowekwa na Idara yake ili kupandisha kiwango cha ufaulu, Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Mji Geita Mwl. Rashid Muhaya amesema kuwa wameazimia kuendesha mafunzo kazini kwa walimu ili kuwaongezea maarifa na ujuzi katika kufundisha, kuendeleza program ya kufundisha masaa ya ziada ili kukamilisha mihtasari ya masomo mapema, kufanya mitihani ya pamoja kwa wanafunzi wa kidato cha pili, nne na sita ili kuongeza ushindani wa shule na shule na kutoa tuzo na zawadi kwa walimu na wanafunzi wanaofanya vizuri katika mitihani ya Taifa.

Kwa upande wa Idara ya Elimu msingi Afisa Elimu Msingi wa Halmashauri ya Mji Geita Bi. Margareth Macha amesema idara yake kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu tumedhamiria kuondoa kabisa tatizo la wanafunzi wasiomudu kujua kusoma,kuhesabu na kuandika kwa kuwapa walimu mbinu na mafunzo mbalimbali  na kufanya tathimini ya maendeleo ya KKK kila mwisho wa mwezi.

Kadhalika Idara ya Elimu msingi imedhamiria kuwahamasisha wazazi na walezi kupitia umoja wa wazazi/walezi na walimu shuleni kuwasaidia wanafunzi kujifunza kwa mwendelezo kuanzia nyumbani ili kuinua viwango vya taaluma. Pia idara itatembelea shule 10 duni mara kwa mara ili kujadili kwa pamoja changamoto zinazowakwamisha na kuzitatua kwa pamoja.

Katika kikao hicho shule zilizofanya vizuri kitaaluma zilipewa zawadi ya vyeti na fedha taslimu sambamba na wanafunzi waliofanya vyema katika mitihani ya kitaifa kama motisha ya kuwafanya wazidi kukazana na kufanya vizuri zaidi kitaaluma,  kadhalika Shule ya Msingi Bung’wangoko ilipewa kinyago kwa kuwa shule ya mwisho kitaaluma .


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa