Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita Ndg. Yefred Myenzi akiambatana na baadhi ya Wakuu wa Idara na Vitengo leo tarehe 03 Juni, 2025 wamefanya ziara ya kutembelea watumishi kwa lengo la kusikiliza changamoto na kukumbushana wajibu wa kila mtumishi
Ziara hii imefanyika katika vituo vitatu; Bung’wangoko Sekondari ikijumuisha watumishi kutoka Kata ya Bung’wangoko, Kasamwa Sekondari ikijumuisha watumishi kutoka Kata ya Kasamwa na Kanyala na Bulela Sekondari ikijumuisha watumishi kutoka Kata ya Shiloleli na Bulela
Mkurugenzi Mtendaji wa Manipsaa amewataka watumishi kufanya kazi kwa ushirikiano na kuheshimiana huku wakizingatia Sheria, Taratibu, Kanuni na Miongozo ya Utumishi wa Umma popote watakapokuwepo.
Huo ni mwendelezo wa utaratibu wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita, akiambatana na wataalamu wa Halmashauri kwa ajili ya kusikiliza na kutatua changamoto za watumishi ambapo kero hizo zinafanyiwa ufumbuzi papo kwa papo.
Timu hiyo kesho tarehe 04 Juni, 2025 iataendelea na ziara katika vituo viwili Shule ya Wasichana Nyankumbu ikijumuisha watumishi kutoka Kata ya Nyankumbu na Mtakuja pamoja na Ukumbi Gedeco wa Halmashauri ikijumuisha watumishi kutoka Kata ya Kalangalala, Buhalahala na Bombambili.
TUFUATILIE KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII
Instagram
Geita Tanzania
Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita
Namba ya Simu: 0282520437
Mobile:
Barua pepe: td@geitatc.go.tz
Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa