• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wekeni Mikakati Madhubuti kutatua Changamoto Zenu- RC Gabriel

Posted on: May 2nd, 2019

Wafanyakazi Jengeni Mikakati ya Kutatua Changamoto Zenu- RC Geita

Mkuu wa Mkoa wa GeitaMhandisi Robert Gabriel amewashauri wafanyakazi katika Mkoa wake kujenga mshikamano katika  kuhakikisha wanatafuta ufumbuzi wa changamoto  mbalimbali zinazowakabili katika utekelezaji wa shughuli zao za kila siku kwenye maeneo yao ya kazi ambazo zipo ndani ya uwezo wao.

Mkuu wa Geita ametoa rai hiyo Tarehe 01 Mei 2019 wakati wa Maadhimisho ya siku ya Wafanyakazi Duniani yaliyofanyika kimkoa katika viwanja vya Shule ya Msingi Chato, wilayani Chato Mkoa wa Geita.

Mhandisi Robert Gabriel ametumia fursa hiyo kuwakumbusha wafanyakazi wote kutimiza wajibu wao kwa kufanya kazi kwa bidii, maarifa, uaminifu na uadilifu na kutendea haki weledi walionao wakiongozwa na miiko ya kazi na taaluma zao.

“Kumbukeni kuwa kutoa huduma kwa wateja wetu ni wajibu wenu hivyo jiepusheni kabisa na kupokea rushwa ya aina yeyote, kwa wale wanaojihusisha na suala la rushwa waache mara moja fanyeni Geita pawe mahala patakatifu” . Aliongeza Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Mhandisi Robert Gabriel  amewatahadharisha Wafanyakazi kuendelea kujikinga na Ugonjwa wa UKIMWI kwa kuwausia kuwa waaminifu, kujizuia na kusubiri pia kila mmoja kujenga utamaduni wa kupima afya kila wakati  ili kufahamu hali zao na kuchukua hatua zinazostahili kupambana na ugonjwa huo. Kadhalika kutowanyanyapaa ndugu na jamaa ambao walioambukizwa bali wawafariji, wawapende, kuwatia moyo na kushiriki pamoja nao katika shughuli za kijamii.

Akibainisha changamoto zinazowakabili Wafanyakazi wa Mkoa wa Geita, Mwenyekitiwa Shirikisho laVyama vya Wafanyakazi Ndugu Ramadhan Pangala amesema kuwa malimbikizo ya madeni, mishahara midogo, ucheleweshwaji wa kupandishwa madaraja na baadhi ya wafanyakazi wa migodini kulipwa mishahara kupitia Serikali za Mitaa na kutokuwa na maduka ya Dawa vijijini kwa ajili ya kuwahudumia wanachama wa Bima ya Afya bado ni changamoto zinazowakabili wafanyakazi wa Mkoa huo.

Ndg. Pangala ametoa rai kwa Serikali kuwahamishia Hazina watumishi wote wanaolipwa mishahara kupitia mapato ya ndani kwani watumishi hao hawapati stahiki yao kwa wakati kama ilivyo kwa watumishi wengine.

Siku ya Wafanyakazi Duniani huadhimishwa Mei mosi kila mwaka kwa lengo la kukumbuka harakati na jitihada zilizofanywa na wafanyakazi wakati wa mapinduzi ya viwanda huko Ulaya. Kwa mwaka huu Madhimisho hayo yalibeba kauli Mbiu isemayo “Tanzania ya Uchumi wa Kati inawezekana, Wakati wa Mishahara na Maslahi kwa Wafanyakazi ni Sasa.”



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa