• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wazazi Waaswa Kuwekeza kwa Watoto

Posted on: June 20th, 2018

Wazazi Waaswa Kuwekeza kwa Watoto

Wazazi na walezi katika Halmashauri ya Mji a Wilaya ya Geita kwa ujumla wametakiwa kutumia raslimali na mali walizonazo kuwaelimisha watoto ili kuwajengea uwezo wangali wadogo katika dhana mbalimbali za uzalishaji mali ili tuweze kuzalisha wataalam wengi wenye tija kwa maslahi ya nchi yetu.

Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Geita Ndugu Herman C. Kapufi wakati wa Maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika yaliyofanyika kiwilaya katika Mtaa wa Nyanguku kata ya Nyanguku, Halmashauri ya Mji wa Geita hivi karibuni.

Mkuu wa Wilaya ya Geita ameongeza kuwa malezi  na makuzi ya watoto ni muhimu katika maendeleo ya nchi lakini wazazi na walezi wengi katika jamii hawatoi fursa ya kutosha kwa watoto ili waweze kutoa mawazo na michango yao katika maamuzi mbalimbali kuanzia ngazi ya familia na jamii kwa ujumla jambo ambalo limewanyima watoto haki yao ya kushiriki.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Nyanguku Mhe. Elias Ngole amewakumbusha wazazi na walezi kuwapenda, kuwalinda na kuwapeleka watoto shule katika umri unaotakiwa. “ Inasikitisha sana kuona watoto wenye umri wa miaka nane hawajapelekwa shule badala yake wanaagizwa na wazazi kwenda kuchunga mifugo. Kulima  na kufanya shughuli mbalimbali za nyumbani.” Aliongeza Mhe. Ngole

Diwani wa Kata ya Nyanguku amewakumbusha wazazi katika kata yake na Kata nyingine za Halmashauri ya Mji wa Geita kuchangia maendeleo ya ujenzi wa madarasa katika Shule za Msingi na Sekondari kwenye maeneo yao na kuwanunulia mahitaji muhimu watoto wao wanaokwenda shule pasipo kusahau jukumu lao la kufuatiliamaendeleo ya kitaaluma  na kinidhamu ya watoto wao wanapokuwa shule.

Watoto wa Shule ya Msingi Nyanguku katika risala yao waliyosoma kwa niaba ya watoto wote wa Halmashauri ya Mji wa Geita wameishukuru Serikali kwa kuwapa elimu bure na chanjo mbalimbali zinazowakinga dhidi ya maradhi. Pia wamewaomba wazazi wa watoto wenye mahitaji maalum kupatiwa haki ya elimu kwa kuandikishwa shule na si kufungiwa majumbani kwani wana haki ya kupata elimu.

Katika Risala ya watoto hao wamewatahadharisha wenzao kujiepusha na mitego ya mali na tamaa inayowavuta kushiriki katika mienendo isiyofaa, Pia wawe wepesi kutoa taarifa katika vyombo mbalimbali vya dola wanapofanyiwa vitendo vya ukatili wa kijinsia. Kadhalika wamewasihi wazazi kuwachukulia watoto wote kama wao kwa kuwazaa hivyo wakemee vitendo vyote vilivyo kinyume na maadili vinavyofanywa na watoto kama kuingia katika kumbi za starehe, muziki na video.

Siku ya Mtoto wa Afrika huadhimishwa Juni 16 kila mwaka barani Afrika kwa lengo la kutekeleza Azimio la Umoja wa Nchi huru za Afrika katika kuwakumbuka watoto wa Kitongoji cha Soweto nchini Afrika ya Kusini waliouwa kinyama tarehe kama hiyo mwaka 1976 wakati wakidai haki yao ya kutokubaguliwa na haki nyingine za msingi zikiwemo kupewa Elimu, huduma za Afya, Kusikilizwa, Kupendwa na kulindwa. Ujumbe wa Mwaka huu ni “Kuelekea Uchumi wa Viwanda: Tusimwache mtoto nyuma”.




Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa