Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita Ndg. Yefred Myenzi, amewataka watumishi wa Manispaa ya Geita kujiepusha na kutuma taarifa ambazo hawana uhakika nazo kwa kuwa ni kinyume cha maadili.
Ndg. Myenzi ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na watumishi wa umma wa Kata ya Nyankumbu na Mtakuja wakati wa ziara yake ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji, kusikiliza na kutatua changamoto zinawazokabili watumishi hao katika utekelezaji wa majukumu yao. Kikao hiko kimefanyika katika shule ya Sekondari ya Wasichana Nyankumbu.
“Nikemee vitendo vya kutumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii ambayo wakati mwingine ina taarifa zisizo rasmi na taarifa za upotoshaji, unavyopost kitu ambacho huna uhakika nacho kuna sheria inayohusiana na mahudhui ya mtandaoni utakabiliana nayo” amesema Myenzi
Ameongezea kusema kuwa watumie mitandao ya kijamii kwa manufaa pasipo kupoteza muda wa mwajiri
“Tutumie mitandao kwa ajili ya manufaa uki-download matirio ya kufundishia, utaalamu wa afya pamoja na mambo mengine ikiwa na kibiashara kuliko kutumia kujifurahisha tu" amesesisitiza Myenzi
Ziara hii mwendelezo wa utaratibu wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita, akiambatana na wataalamu wa Halmashauri kwa ajili ya kusikiliza na kutatua changamoto za watumishi ambapo kero hizo zinafanyiwa ufumbuzi papo kwa papo. Kwa leo pia timu imekutana na watumishi wa Kata ya Kalangalala, Buhalahala na Bombambili katika Ukumbi Gedeco.
Timu hiyo kesho tarehe 05 Juni, 2025 itaendelea na ziara katika Kata za Ihanamilo, Nyanguku na Mgusu.
TUFUATILIE KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII
Instagram
Geita Tanzania
Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita
Namba ya Simu: 0282520437
Mobile:
Barua pepe: td@geitatc.go.tz
Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa