• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

WATUMISHI GEITA MJI WANUFAIKA NA MAFUZO YA TAHADHARI NA KINGA DHIDI YA MAJANGA YA MOTO

Posted on: August 12th, 2024

Kampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya GGML iliyopo mkoani Geita, kwa kushirikiana na Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Geita imetoa mafunzo kwa watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Geita juu ya kukabiliana na majanga ya moto.

Akitoa mafunzo hayo leo Agosti 12, 2024 katika Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya mji wa Geita, Kaimu kamanda wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Geita Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Edward Lukuba ameipongeza GGML kwa kuendelea kuiishi dhana yao ya usalama na kueleza kuwa wamekuwa mstari wa mbele kuhamasisha Jamii kuzingatia usalama huku akisisitiza kuwa jukumu la kujikinga na majanga ya moto ni la kila mmoja kwenye jamii.

Mrakibu Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Edward Lukuba akifafanua jambo kwa Watumishi wa Halmashauri.

Bw. Lukuba amesema, anaipongeza GGML kwa kuja na mkakati huo madhubuti wa kutoa mafunzo haya kwa watumishi mbalimbali waliopo katika jengo la Makao Makuu ya Halmashauri. Na anaamini hapo hajatoa elimu kwa watumishi hao tu bali anaamini elimu hiyo itafika hadi majumbani kwa watumishi hao na itasaidia kufanya watu kujikinga na majanga ya moto.

Awali GGML ilitoa mafunzo kwa wanafunzi ambapo jumla ya wanafunzi waliopata elimu shule za sekondari ni 15,091 na walimu 2 kwa halmashauri ya mji na wilaya ya Geita, kama anavyobainisha Kaimu Afisa Elimu Sekondari Bi. Linda Marandu.

Baadhi ya Watumishi wa Halmshauri ya Mji wakiwemo Bw. Justine Mbilinyi na Bi. Valerian Makonda wamesema kuwa mafunzo hayo yamewapa mwanga juu ya kuweza kuchukua tahadhari kuhusu majanga ya moto sio tu hapo ofisini katika jengo la Halmashauri lakini pia hata majumbani ambapo mara nyingi hatari ya moto hutokea na huwa wanashindwa kutoa msaada.

Mtumishi wa Halmashauri ya Mji Geita akifanya Majaribio ya kuzima moto kwa vitendo.

Naye, Bw. Mussa Mbyana akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mji ametoa shukrani kwa GGML na Jeshi la zimamoto na uokoaji kwa kuandaa mafunzo hayo ambayo yatatusaidia katika kazi zetu za kila siku na amewaomba mafunzo haya yasiishie tu hapa Makao Makuu bali yawafikie na watumishi waliopo nje ya mji na hata jamii kwa ujumla.

Mafunzo yaliyotolewa ni sehemu ya mipango ya GGML katika kuchangia maendeleo ya jamii ambapo wamekuwa wakishirikiana na taasisi nyingine za serikali na mashirika yasiyo ya kiserikali ili kuhakikisha kuwa jamii inakuwa salama na yenye ustawi kwa Jamii na Taifa kwa ujumla.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa