Ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa ya Geita imewataka Watumishi wa Umma kutimiza majukumu yao kwa kuzingatia Sheria, Kanuni na Taratibu huku wakisistizwa kutambua haki zao za msingi wanazostahili kama Watumishi wa Umma.
Akiwasilisha maelekezo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Manispaa, Mkuu wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimaliwatu Bi. Ellah Makese ametoa kauli hiyo leo tarehe 05 June 2025 wakati wa kikao kazi na Watumishi wa Kata ya Ihanamilo na Nyanguku kilichofanyika katika shule ya Sekondari Ihanamilo.
“Kanuni za maadili ndizo ambazo zinazotufanya sisi tuwe watumishi wa Umma na hizo ndizo zinazotufanya sisi tukamilike, ukikiuka hizo kanununi za maadili maana yake wewe utakuwa ume-misbehavior” amesema Ellah
Ziara hiyo ya kikazi iliyolenga kuhimiza uwajibikaji, kusikiliza na kutatua changamoto zinawazokabili watumishi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa lengo la kuboresha utendaji kazi kwa Watumishi wa Manispaa.
Amesema ni wajibu wa kila Mtumishi kutambua haki zake ikiwemo stahili zake kama Mtumishi wa Umma pamoja na likizo huku akisisitiza haki lazima iende sambamba na kutimiza wajibu wa kutoa huduma bora.
Aidha amewataka watumishi kuwa n vyanzo vingine vya mapato tofauti na mshahara ili hata wanapomaliza utumishi wao Serikalini tayari wanakuwa wameshajikita katika jambo fulani na hii itawaepushia kukurupuka kuingia kwenye mikopo mingi inayopelekea kuanguka kiuchumi na wakati mwingine kuwasababishia msongo wa mawazo au vifo vya mapema
Naye Bw. Kadole Ngumungu, Afisa Utumishi akiwasilisha mada juu ya Kanuni za Utumishi wa Umma amewataka watumishi kuzingatia masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na nidhamu katika utumishi wa umma na utendaji kazi kiufanisi ili kuleta tija katika kazi zao.
Pia, amewataka watumishi kuimarisha ushirikiano na mawasiliano mahali pa kazi katika kutekeleza majukumu yao.
Timu hiyo imefikia tamati ya ziara yake leo kwa kutembelea pia watumishi wa Kata ya Mgusu.
TUFUATILIE KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII
Instagram
Geita Tanzania
Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita
Namba ya Simu: 0282520437
Mobile:
Barua pepe: td@geitatc.go.tz
Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa