• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Watoto wa Kike Watakiwa Kujitambua

Posted on: October 12th, 2023

Watoto wa Kike Watakiwa Kujitambua

Afisa Elimu awali na msingi wa Halmashauri ya Mji Geita Bi. Margareth Macha amewausia Watoto wa kike kujitambua thamani zao na umuhimu wao katika jamii siku zote, ili kuepukana na mimba za utotoni, maradhi na vitendo vinavyovunja maadili ya kitanzania.

Bi. Macha ametoa ushauri huo tarehe 11 Oktoba 2023 alipokuwa akihutubia hadhara ya Watoto kutoka shule mbalimbali za msingi na sekondari walioshiriki maadhimisho ya Siku ya mtoto wa kike yaliyofanyika kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Nyanza Geita mjini.

Afisa Elimu msingi aliongeza kuwa chanzo cha tatizo la watoto wengi kukatishwa masomo  ni Watoto wenyewe wa kike kukubali kurubuniwa kwa vishawishi mbalimbali ikiwemo chips, mayai, nyama choma, soda pamoja na vizawadi vidogo.

“Kadhalika baadhi ya Watoto wa kike wameshindwa kuendelea na shule kutokana na changamoto za kifamilia ikiwemo kutengana kwa wazazi kunakopelekea Watoto kukosa malezi na uangalizi wa karibu wa wazazi/walezi. Hivyo wazazi na walezi timizeni wajibu wenu katika malezi ili tuwasaidie Watoto wetu wa kike kutimiza ndoto zao.” Aliongeza Bi. Margareth Macha.

Bi. Macha ametoa wito kwa wenyeviti wa mitaa pamoja na watendaji wote wa Serikali kuanzia ngazi ya vitongoji kuhakikisha wanawakamata watu wote ambao wamejenga tabia ya kutelekeza familia kwa kisingizio cha ugumu wa Maisha.

Msimamizi wa masuala ya jinsia kutoka mradi wa KAGIS ulioko chini ya Shirika la Plan International Bi. Hildergada Mashauri amesema uwepo wa mradi wa kutetea mtoto wa kike umeisaidia jamii kuondokana na dhana potofu ya kumuona mtoto wa kike kama kiumbe dhaifu asiye na uwezo wa kuwa kiongozi na hivyo kutotoa kipaumbele cha elimu kwa Watoto wa kike.

Siku ya mtoto wa kike duniani huadhimishwa Oktoba 11 kila mwaka kwa lengo la kuwakumbusha Watoto wa kike juu ya wajibu wao katika jamii na umuhimu wao katika kujitambua na kuepukana na vitendo viovu vitakavyowakwamisha kutofikia ndoto zao. Pia kuendelea kuwasisitiza wazazi juu ya malezi ya Watoto wao. Kwa mwaka 2023 maadhimisho hayo yalibeba kauli mbiu isemayo “Haki zetu ni hatima yetu, Wakati ni sasa.”


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa