• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Watendaji Watakiwa Kusimamia Vyema Mkataba Wa Lishe

Posted on: October 28th, 2022

Watendaji Watakiwa Kusimamia Vyema Mkataba Wa Lishe

Watendaji wa Kata 13 za Halmashauri ya Mji wa Geita wameagizwa kuhakikisha wanasimamia kikamilifu utekelezaji wa viashiria vyote vilivyomo katika mkataba wa lishe ili kuleta mabadiliko katika kuboresha hali ya lishe kuanzia ngazi ya kaya hadi jamii nzima pamoja na kuweka utaratibu maalum wa kuadhimisha siku ya lishe kwa kila kata.

Agizo hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Ndugu Zahara Michuzi hivi karibuni alipokuwa akishuhudia tukio la watendaji wote wa kata kusaini mkataba wa lishe, tukio lililofanyika katika ukumbi wa mikutano katika jengo la ofisi ya Halmashauri ya Mji Geita eneo la Magogo Geita mjini.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita ameeleza kuwa viashiria vinavyotakiwa kutekelezwa ni pamoja na Watoto kupatiwa chakula mashuleni, wakina mama wajawazito kuhudhuria kliniki ipasavyo na kupatiwa madini joto, Watoto kupatiwa vitamin A, Watoto wenye utapiamlo mkali kupatiwa huduma vituoni na utoaji wa fedha ipasavyo kwa ajili ya afua za lishe.

“Watendaji wote hakikisheni mnasimamia vigezo vya upimaji na vipaumbele vya kata kwa kila mwaka ambavyo ni upatikanaji wa taarifa za hali ya lishe kwa Watoto chini ya miaka mitano, kufanya ufuatiliaji wa Watoto walioacha matibabu ya utapiamlo kwa kushirikiana na watoa huduma za afya ngazi ya jamii.” Aliongeza Bi. Zahara Michuzi.

Kwa upande wake Afisa Lishe wa Halmashauri ya Mji Geita Oscar Obeid amesema kuwa ataendelea kujipanga Zaidi ili kuhakikisha kata zote ndani ya Halmashauri kila kiashiria kinafika asilimia 95 na sio chini ya hapo. Kadhalika kitengo chake kitaendelea kutoa elimu kwa jamii ili wazazi watambue umuhimu wa kuchangia chakula cha Watoto mashuleni ili kukuza kiwango chao cha lishe, kuongeza usikivu na kupunguza tatizo la utoro kwa wanafunzi.

Utekelezaji wa mkataba wa lishe uliosainiwa utakuwa wa miaka nane kuanzia tarehe mosi Julai 2022 hadi tarehe 30 Juni 2030 kulingana na malengo na shabaha zilizoainishwa katika mikakati ya kitaifa ya muda mfupi, muda wa kati pamoja na muda mrefu ambayo ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo yam waka 2025, mpango wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano pamoja na Ilani ya Uchaguzi ya Chama Tawala na Sera mbalimbali za nchi.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa