• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Nyuki na Misitu
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Wanufaika Washauriwa Kuanzisha Viwanda Vidogo

Posted on: December 27th, 2022

Wanufaika Washauriwa Kuanzisha Viwanda Vidogo

Jumla ya vikundi 33 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ambao wamenufaika na mikopo isiyo na riba ambayo imetolewa na Halmashauri ya Mji Geita wameshauriwa kutumia fedha hizo kwa kuanzisha viwanda vidogo na kubadilika kutoka kwenye biashara zilizozoeleka na zinafanywa na watu wengi kwenye jamii.

Akiongea wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya hundi za mkopo kwa walengwa katika ukumbi wa Eneo maalum la uwekezaji kiuchumi Bombambili mjini Geita hivi karibuni, Mbunge wa Geita mjini Mheshimiwa Costantine Kanyasu amewasisitiza wanufaika wa mkopo kuanzisha viwanda vidogo ili kuzipa thamani bidhaa zao akitolea mfano wa mafundi cherehani ambao wanaweza kukuza bishara yao na kuwa kiwanda kidogo.

“Wanavikundi mlionufaika na mikopo kutoka Serikalini hakikisheni mnaitumia mikopo hiyo kwa malengo ambayo yamekusudiwa ili kujiletea maendeleo yenu binafsi na jamii kwa ujumla na sio kutumia fedha hizo katika shughuli za sherehe za Noeli na Mwaka mpya.” Aliongeza Mhe. Kanyasu.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Wilson Shimo amewatahadharisha wanufaika wa mikopo hiyo kuacha tabia ya kutorejesha mikopo kwa wakati mpaka wanafikishwa kwenye vyombo vya dola jambo ambalo linasababisha usumbufu usio na tija, bali wanapozalisha mikopo yao ndipo wanawawezesha na wenzao walioomba mikopo kupatiwa kwa wakati muafaka katika awamu nyingine.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri, Afisa vijana wa Halmashauri ya Mji wa Geita amesema kuwa jumla ya vikundi 33 vikiwemo 18 vya wanawake, 11 vya vijana na 4 vya watu wenye ulemavu vimepatiwa shilingi Milioni 387 kwa ajili ya kuendeleza shughuli zao za kiuchumi. Ndg. Zengo amefafanua kuwa katika mwaka wa fedha 2022/2023 jumla ya kiasi cha shilingi 906,628,800 ikiwa ni asilimia 10 ya mapato ya ndani kimetengwa kwa ajili ya utoaji mikopo kwa makundi maalum. Pia Halmashauri imeweza kukusanya shilingi 488,694,700 ambazo ni mikopo chechefu.


Matangazo

  • TANGAZO LA URASIMISHAJI WA MAKAZI YASIYOPANGWA January 16, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI July 22, 2022
  • TANGAZO LA KAZI ZA MACHINJIO August 16, 2022
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA GEITA MJI December 02, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • Kamati Ya Siasa Wilaya Ya Geita Yaridhishwa na Miradi Geita Mji

    January 26, 2023
  • Walimu 668 Geita Mji Wanufaika na Vishikwambi

    January 18, 2023
  • Wanufaika Washauriwa Kuanzisha Viwanda Vidogo

    December 27, 2022
  • Timu Ya Halmashauri Yapata Udhamini Kutoka GGM

    December 20, 2022
  • Zaidi

Video

Machinjio ya Kisasa Mpomvu Yaanza kazi
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Applications Forms
  • Acts
  • Barua pepe za watumishi
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa