• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wanawake Watakiwa Kuwa Vinara Kupinga Ukatili

Posted on: March 10th, 2023

Wanawake Watakiwa Kuwa Vinara Kupinga Ukatili

Wanawake waishio katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Mji wa Geita wametakiwa kuwa mstari wa mbele katika kupinga vitendo vya kikatili vinavyoendelea kushamiri kila kukicha katika jamii yao wanamoishi ili kujenga Geita yenye upendo, kuthamini utu na heshima ya kila mmoja kulingana na jinsia yake.

Wito huo umetolewa hivi karibuni na Mbunge wa Geita Mjini Mheshimiwa Costantine Kanyasu alipomwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Geita katika kongamano kubwa la Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani lililofanyika katika ukumbi wa Gedeco na kujumuisha makundi mbalimbali ya wanawake.

Mhe. Kanyasu ameeleza kuwa awali ya yote wanawake wanatakiwa kupendana kwa kusaidiana na kukwamuana kiuchumi kupitia vikundi vya kijamii vya kuweka na kukopa, kujiunga na vikundi vinavyopatiwa mikopo isiyo na riba kutoka Serikalini na mikopo yenye riba nafuu inayotolewa na taasisi mbalimbali za kifedha.

Katika kuadhimisha kilele cha siku ya wanawake Duniani, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Ndg. Zahara Michuzi kwa niaba ya wanawake wote wa Halmashauri hiyo amekabidhi vifaa visaidizi kwa wanafunzi Neema Katwale wa Shule ya Sekondari Kisesa, Fatuma Fadhili wa Shule ya Sekondari ya wasichana Nyankumbu na Justin Magaka wa Shule ya Sekondari Kasamwa wakiwakilisha wanafunzi wengine wenye mahitaji maalum katika Mji wa Geita

Kwa upande wa mwanafunzi aliyepatiwa msaada Bi. Neema Katwale ametoa shukrani za dhati kwa watumishi wa Makao makuu ya halmashauri ya Mji Geita kwa kuona umuhimu wake binafsi na wenzao ambao wanahitaji vifaa visaidizi katika Maisha yao ya kila siku.

Siku ya Wanawake Duniani huadhimishwa tarehe 8/03 kila mwaka kwa lengo la kuenzi mchango unaofanywa na wanawake katika njanya mbalimbali zikiwemo za taasisi ,Serikali na binafsi. Mbegu za siku hii zilipandwa mwaka wa 1908 wakati wanawake 15,000 walipoandamana katika jiji la New York wakidai kupunguziwa masaa ya kufanya kazi, mishahara bora na haki ya kupiga kura.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa