• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wanawake Wahimizwa Kupinga Ukatili

Posted on: March 8th, 2024

Wanawake Wahimizwa Kupinga Ukatili

Wanawake katika Halmashauri ya Mji Geita wamehimizwa kupinga vitendo vya kikatili kwa kutoa taarifa sahihi juu ya matukio ya ukatili yanayoendelea katika jamii na kujilinda wao wenyewe, Watoto na kuepuka kufanya ukatili dhidi ya Watoto wanaowalea.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Tawala Wilaya ya Geita Ndugu Lucy Beda alipomwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Geita katika maadhimisho ya Siku ya wanawake duniani yaliyofanyika katika ngazi ya Halmashauri kwenye viwanja vya EPZ Bombambili tarehe 07/03/2024.

Ndugu Lucy Beda ametumia wasaa huo kuwakumbusha wanawake ambao wanajihusisha na vitendo vya kikatili kama kutupa Watoto baada ya kuzaliwa, kuwanyanyasa Watoto wa kufikia na kuwapiga hadi kujeruhi waume zao waache mara moja vitendo hivyo ambavyo ni kinyume na maadili ya mtanzania na vitawapelekea kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

“Wanawake msinyamaze juu ya ukatili wa kijinsia unaoendelea majumbani kwenu ambao mara nyingi unafanywa na jamaa zenu, ndugu zenu na majirani, pazeni sauti ili kupinga vitendo hivyo vitakavyowakwamisha Watoto wenu kukatishwa malengo yao. Kadhalika msiache  majukumu yote ya malezi ya Watoto kwa mabinti wasaidizi wa kazi ili kujenga urafiki baina yenu na Watoto.’’ Ameongeza Katibu Tawala Wilaya ya Geita.

Akisoma risala kwa niaba ya wanawake wote wa Halmashauri ya Mji Geita Bi. Devotha Anthony amesema kuwa wanaiomba Serikali ya awamu ya sita kurejesha utaratibu wa utoaji wa mikopo isiyokuwa na riba ili wanawake, vijana, watu wenye ulemavu na mtu mmoja mmoja waweze kukuza mitaji yao na kuendeleza shughuli za kiuchumi kwa lengo la kujikwamua wao binafsi na familia zao.

Afisa Maendeleo ya jamii Bi. Valeria Makonda ameeleza kuwa Halmashauri ya Mji Geita ina kamati za kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto ambazo hushughulikia masuala yote ya ukatili kwa wanawake na watoto kuanzia ngazi za mitaa, vijiji, kata mpaka ngazi ya Halmashauri. Kamati hizo hufanya kazi kwa kushirikiana na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali pamoja na taasisi mbalimbali kama NELICO, VSO, AICT na Plan International zinazojishughulisha na maswala ya kupinga ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Siku ya wanawake Duniani huadhimishwa kila mwaka kwa lengo la kupima na kutathimini kiasi cha utekelezaji wa malengo na maazimio mbalimbali ya kitaifa na kimataifa na kusaidia kujenga na kuimarisha mshikamano wa wanawake duniani ni nafasi pia ya kuona juhudi mbalimbali zinazofanywa katika kumuendeleza mwanamke na kufanya uhamasishaji wa jamii  kuhusu utekelezaji wa sera, mipango na ahadi za Serikali katika kudumisha amani na usawa wa kijinsia.

Maadhimisho ya mwaka 2024 yamebebwa na Kauli Mbiu isemayo ‘ Wekeza kwa Mwanamke Kuharakisha Maendeleo ya Taifa na Ustawi wa Jamii ’.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI WAKUMBUSHWA KUFANYA KAZI KWA UMOJA

    June 30, 2025
  • BONAZA LA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA

    June 28, 2025
  • WANANCHI WA MANISPAA YA GEITA WAKUMBUSHWA KUENDELEA KUFANYA USAFI

    June 28, 2025
  • DC KOMBA AWAKARIBISHA NACHINGWEA KUJIFUNZA UCHIMBAJI GEITA, ATOA USHAURI WA NAMNA NZURI YA USIMAMIZI WA MIGODI

    June 26, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa