• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wananchi Watakiwa Kuunga Mkono Juhudi za Serikali

Posted on: November 7th, 2023


Wananchi Watakiwa Kuunga Mkono Juhudi za Serikali

Wananchi katika Mkoa wa Geita wametakiwa kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanya kazi kwa bidii ili dhamira ya dhati ya Serikali inayolenga kuleta maendeleo kwa kila mtanzania iweze kutimizwa.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mheshimiwa Martine Shigela hivi karibuni alipofanya ziara ya kikazi kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Mji Geita kupitia fedha zilizotolewa na Serikali kuu pamoja na fedha kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akizungumza alipokuwa akitembelea mradi wa ujenzi wa Shule maalum ya wasichana katika mkoa wa Geita ambayo inajengwa katika Kata ya Bombambili Halmashauri ya Mji Geita Mhe. Shigela amewaagiza watendaji wote wa Serikali kuanzia ngazi ya mtaa ambao wanasimamia ujenzi wa mradi huo kushirikiana kikamilifu kuhakikisha mradi huo unajengwa katika ubora wa hali ya juu na unakamilika kwa wakati.

Mkuu wa Mkoa wa Geita pia ameziagiza taasisi za huduma ya umeme, maji, Barabara kuanza kufanya tathimini ya uwekaji wa huduma hizo katika mradi wa Shule maalum ya wasichana ili ifikapo mwezi Januari 2024 wakati wa ufunguzi rasmi wa shule hiyo wanafunzi watakaochaguliwa kujiunga katika shule hiyo wasipate shida ya kukosekana kwa huduma hizo muhimu.

Mwenyekiti wa mafundi wazawa wanaojenga mradi huo Mhandisi Robert Gabriel ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuwaamini na kuwapatia kazi ya ujenzi wa mradi huo ambao umewawezesha kupata fursa ya kupata riziki kwa ajili yao binafsi na familia zao. Pia mafundi hao wamejipanga kujenga majengo yenye ubora wa hali ya juu na kumaliza kazi kwa wakati ili mwezi Januari 2024 shule hiyo iweze kupokea wanafunzi.

Miradi iliyotembelewa na kukaguliwa na Mkuu wa Mkoa wa Geita ni pamoja na ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kata Nyantorotoro katika Kata ya Nyankumbu ambao unajengwa kwa Shilingi 584,280,028 kutoka Serikali kuu, Ujenzi wa jengo la wagonjwa wa nje, nyumba pacha ya mganga, kichomea taka, choo cha matundu manne  katika Zahanati ya Shinamwendwa Kata ya Nyanguku iliyojengwa kwa Shilingi 231,860,000 za mapato ya ndani, mfuko wa jimbo na nguvu za wananchi pamoja na ujenzi wa Shule maalum ya Sekondari ya wasichana Geita mjini ambayo inajengwa kwa Shilingi Bilioni 3 kutoka Serikali kuu.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa