• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wananchi Wakumbushwa Kupima VVU

Posted on: December 4th, 2023

Wananchi Wakumbushwa Kupima VVU

Wananchi mkoani Geita wameshauriwa kujijengea utamaduni wa kupima Virusi vya UKIMWI mara kwa mara ili kutambua afya zao na kujifunza namna bora ya kuishi na maambukizi ili kujenga afya bora ya mwili na kuzuia maambukizi mapya kutoongezeka.

Kauli hii imetolewa hivi karibuni na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mheshimiwa Martine Shigela alipokuwa akihutubia wananchi waliojitokeza katika Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani yaliyofanyika Disemba mosi katika viwanja vya CCM Kalangalala Geita mjini.

Mkuu wa Mkoa wa Geita amewaeleza wananchi kuwa UKIMWI bado upo na takwimu zinaonesha kuwa maambukizi ya ugonjwa huo katika mkoa wa Geita  bado yako juu kwa asilimia 4.7%  ambapo wanawake wanaongoza kwa asilimia 60.7%,  hivyo kuna umuhimu wa kila mwananchi kutambua afya yake na kuchukua tahadhari.

“Ugonjwa wa UKIMWI unaepukika, mtu anaweza kujikinga asipate maambukizi na wenye maambukizi wafuate kanuni bora za kuishi kwa kula chakula bora chenye vitamin zote na matunda pamoja na kutumia kikamilifu dawa za kufubaza makali ya Virusi vya UKIMWI ili watu hao waweze kupata nguvu za kutimiza majukumu yao na hatimaye kutimiza malengo waliyojiwekea.” Aliongeza Mhe. Martine Shigela.

Mkuu wa Mkoa wa Geita ametumia fursa hiyo kuwaasa wauguzi, madaktari na wahudumu wote wa afya kuwapenda wagonjwa wa UKIMWI na wenye VVU ili waone kwamba kupata ugonjwa huo sio mwisho wa Maisha, kadhalika jamii haipaswi kuwanyanyapaa waathirika wa VVU kwa sababu wao ni watu wa muhimu sana katika jamii.

Akiwasilisha mikakati waliyojipangia kama mkoa, Mratibu wa UKIMWI Mkoa Ndg. Last Lingston amesema kuwa Serikali mkoani Geita kwa kushirikiana na wadau wamejipanga kuendelea kuielimisha jamii juu ya tahadhari dhidi ya maambukizi mapya ya VVU, Kuwahamasisha waajiri kutenga bajeti za mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI kwenye mipango na kutoa fedha za utekelezaji pamoja na kuwashirikisha viongozi wa kidini ili kuongeza hamasa kwa wanaume kujitokeza kupima VVU na kupunguza unyanyapaa na ukatili wa kijinsia kwa Watoto.

Maadhimisho ya mwaka 2023 yalikuwa na Kauli mbiu isemayo “JAMII IONGOZE KUTOKOMEZA UKIMWI” ikisisitiza kuimarisha ushirikishwaji wa jamii kupitia Asasi za kiraia katika kuongoza mwitikio wa mapambano dhidi ya VVU na UKIMWI kwa kuhakikisha huduma za VVU na UKIMWI zinayafikia makundi mbalimbali kwenye jamii.











Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA KOZI YA AWALI YA JESHI LA AKIBA WAPATIWA ELIMU YA HABARI

    July 04, 2025
  • WATUMISHI WAKUMBUSHWA KUFANYA KAZI KWA UMOJA

    June 30, 2025
  • BONAZA LA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA

    June 28, 2025
  • WANANCHI WA MANISPAA YA GEITA WAKUMBUSHWA KUENDELEA KUFANYA USAFI

    June 28, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa