• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

WANANCHI WA MKOA WA GEITA WATAKIWA KUWA WASAFI

Posted on: January 29th, 2022

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Innocent Bashungwa ametoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Geita kuwa sehemu ya mfano kwa kuzingatia usafi katika mazingira yanayowazunguka kwa hiari.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Innocent Bashungwa (aliyesimama juu ya kiti),akizungumza wakati akizindua  Kampeni ya usafi wa mazingira uliofanyika leo Januari 29,2022 Mkoani Geita.

Waziri Bashungwa ametoa wito huo leo Januari 29, 2022 wakati akizindua wa Kampeni ya usafi wa mazingira Mkoa wa Geita na kauli mbiu ya “Usafi wa Geita ni wajibu wangu, Mazingira bora ni ni fahari yangu”

“Utaratibu mliouweka kila wiki kufanya usafi mshirikiane na makapuni yanayochimba dhahabu hapa Geita na wadau wengine kuhakikisha tunakuwa na Geita safi inayomelemeta” amesema Bashungwa

Aidha, Waziri Bashungwa amewataka wasafiri wote kubadilika kwani kuna baadhi ya watu wanapanda daladala na mabasi ya kwenda mikoa wakimaliza kunywa soda na biskuti au kitu chochote kilicho kwenye mfuko au chupa wakimaliza kutumia wanatupa dirishani kitu ambacho ni uvunjifu wa sheria ya mazingira na sheria za usalama barabarani hivyo tunapaswa kubadiika ili kuweka mazingira safi.

Pia, Waziri Bashungwa amemuelekeza Mkuu wa Wilaya ya Geita Mjini kushirikiana na na Baraza la madiwani kuweka mikakati ya kuboresha stendi ya mkoa ili kuwa na stendi bora na ya kisasa inayotambulisha Mkoa wa Geita.

Nae, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Rosemary Senyamule ameeleza kuwa wamekubaliana na wananchi kuhakikisha kila mtu anatunza mazingira katika eneo lake ambapo zoezi la kufanya usafi litakuwa endelevu na litafanyika kila Jumamosi ya kila wiki na kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi zoezi hili litafanyika kwa pamoja kama leo hii.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Rosemary Senyamule, akizungumza wakati wa uzinduzi wa Kampeni ya usafi wa mazingira uliofanyika leo Januari 29,2022 Mkoani Geita.

Uzinduzi wa Kampeni hiyo ya usafi ni utekelezaji wa Maelekezo ya Waziri Bashungwa aliyoyatoa kwa Wakuu wa Mikoa pamoja na Wakuu wa Wilaya zote nchini kuhakikisha wanasimamia suala zima la usafi hususani katika miradi yote ya barabara, masoko na stendi.

Katika uzinduzi huu Taasisi mbalimbali za kiserikali, binafsi na za dini pamoja na wananchi zimeungana katika kuhakikisha zoezi hili linafanikiwa zikiwemo vyombo vya Ulinzi na usalama, Mamlaka ya mapato Tanzania, Shirikia la Umeme, RUWASA, TARURA, GGML, GEUWASA, CRDB Bank, NMB Bank, NBC Bank, shirika la Posta Tanzania, Plan International na Madhehebu mbalimbali ya Dini.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WATUMISHI WAKUMBUSHWA KUFANYA KAZI KWA UMOJA

    June 30, 2025
  • BONAZA LA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA

    June 28, 2025
  • WANANCHI WA MANISPAA YA GEITA WAKUMBUSHWA KUENDELEA KUFANYA USAFI

    June 28, 2025
  • DC KOMBA AWAKARIBISHA NACHINGWEA KUJIFUNZA UCHIMBAJI GEITA, ATOA USHAURI WA NAMNA NZURI YA USIMAMIZI WA MIGODI

    June 26, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa