• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wananchi Geita Wapongezwa Kujitoa Kuchangia Miradi

Posted on: May 14th, 2020

Wananchi Geita Wapongezwa Kujitoa Kuchangia Miradi

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ametoa pongezi za dhati kwa wananchi wa kata zote za Halmashauri ya Mji Geita kwa kujitoa kifedha na nguvukazi katika kuchangia miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwenye maeneo yao hususan ujenzi wa vyumba vya madarasa na zahanati.

Mkuu wa Mkoa wa Geita ametoa pongezi hizo hivi karibuni alipokuwa katika ziara ya kuweka mawe ya msingi kwenye baadhi ya Shule za Msingi na Sekondari pamoja na Zahanati zilizojengwa na Halmashauri ya Mji kwa kushirikiana na wananchi wa maeneo hayo pamoja na fedha za wahisani kama Mgodi wa Dhahabu wa Geita.

Mhandisi Robert Gabriel ameongeza kuwa wananchi ambao wamejitoa na wanaendelea kujitoa kwa hali na mali katika ujenzi wa miundombinu mbalimbali wanastahili kupongezwa na kuhamasishwa waendelee na moyo huo  kadhalika viongozi wa Serikali kuanzia ngazi ya mtaa na vijiji mnatakiwa kuacha kupiga porojo na kutumia raslimali fedha zilizopo kuunganisha nguvu kwa pamoja ili kuleta mabadiliko makubwa katika sekta muhimu kama Afya, Elimu na Barabara.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Mji Geita Ndg. Rashid Muhaya amesema kuwa ujenzi wa Shule ya Sekondari Lukaranga utasaidia kupunguza idadi ya wanafunzi watoro ambao walikuwa wakibaki nyumbani kutokana na kuchoka kutembea umbali mrefu kwenda shule ya Sekondari Kivukoni umbali wa zaidi ya kilomita tano.

Katika ziara yake ambayo ililenga kuhamasisha jitihada za wananchi katika kuchangia ujenzi wa miradi ya maendeleo, Mkuu wa Mkoa wa Geita aliweka mawe ya msingi katika Shule za Sekondari Lukaranga iliyoko katika Kata ya Nyankumbu na Bombambili, Shule ya Msingi Uwanja katika Kata ya Nyankumbu pamoja na Zahanati ya Ikulwa iliyoko Kata ya Ihanamilo zikiwakilisha miradi yote ambayo imejengwa kwa ushirikiano baina ya Serikali na wananchi.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa