• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Nyuki na Misitu
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Wananchi Geita Wahimizwa Kutunza Miti

Posted on: December 8th, 2022

Wananchi Geita Wahimizwa Kutunza Miti

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mheshimiwa Wilson Shimo amewasisitiza wananchi wilayani kwake kuhakikisha wanaitunza miti iliyopandwa na itakayoendelea kupandwa katika maeneo mbalimbali ya makazi, maofisini, shuleni na pembezoni mwa barabara.

Mhe. Shimo ametoa rai hiyo Tarehe 08/12/2022 alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa Shule ya msingi Mbugani aliposhiriki zoezi la upandaji miti katika shule hiyo ikiwa ni sehemu ya kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Juma la Uhuru wa Tanzania Bara hapo tarehe 9 Disemba 2022.

Mkuu wa Wilaya ya Geita ameeleza kuwa kwa kupanda na kutunza miti ni sehemu ya utunzaji mazingira kadhalika zoezi la upandaji miti katika juma la Uhuru ni historia kwa vizazi vijavyo ambapo watakuwa wanakumbuka matukio yaliyofanyika wakati wa maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru katika Wilaya ya Geita kwa mwaka 2022.

Mhe. Shimo amewaeleza wananchi wa Wilaya ya Geita pamoja na watumishi wa taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi kujenga desturi ya kupanda miti kwa wingi katika maeneo yao ili kupata faida za miti ikiwa ni pamoja na kuwapatia matunda, kivuli, mbao pia kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kurudisha uoto ulioharibiwa.

Kwa upande wake Kaimu Mhifadhi misitu Wilaya ya Geita Ndg. Sandusy C. Nguyale ameeleza kuwa katika Maadhimisho ya juma la miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara jumla ya miti 12,550 imepandwa katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Geita na ameendelea kuwahimiza wananchi na taasisi mbalimbali za Umma na binafsi Kwenda kuchukua miche ya miti katika kitalu cha Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) kilichopo eneo la Usindakwe Kata ya Buhalahala Geita mjini na kupanda katika maeneo yao ili kufikia malengo ya kupanda miti 1,500,000 kwa mwaka 2022/2023.

Maadhimisho ya juma la Uhuru wa miaka 61 ya Tanzania Bara yanayoongozwa na kauli isemayo “Miaka 61 ya Uhuru Amani na umoja ni nguzo kwa Maendeleo yetu.” Wilayani Geita yamepambwa kwa shughuli mbalimbali zikiwemo usafi wa mazingira katika maeneo ya masoko, shuleni na kwenye makazi ya watu, upandaji miti, mashindano ya michezo mbalimbali kwa wanafunzi, midahalo na kutembelea shule ya wanafunzi wenye mahitaji maalum Mbugani pamoja na wafungwa katika gereza la Geita


Matangazo

  • TANGAZO LA URASIMISHAJI WA MAKAZI YASIYOPANGWA January 16, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI July 22, 2022
  • TANGAZO LA KAZI ZA MACHINJIO August 16, 2022
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA GEITA MJI December 02, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • Kamati Ya Siasa Wilaya Ya Geita Yaridhishwa na Miradi Geita Mji

    January 26, 2023
  • Walimu 668 Geita Mji Wanufaika na Vishikwambi

    January 18, 2023
  • Wanufaika Washauriwa Kuanzisha Viwanda Vidogo

    December 27, 2022
  • Timu Ya Halmashauri Yapata Udhamini Kutoka GGM

    December 20, 2022
  • Zaidi

Video

Machinjio ya Kisasa Mpomvu Yaanza kazi
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Applications Forms
  • Acts
  • Barua pepe za watumishi
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa