• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wananchi Geita Wahimizwa Kutunza Miti

Posted on: December 8th, 2022

Wananchi Geita Wahimizwa Kutunza Miti

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mheshimiwa Wilson Shimo amewasisitiza wananchi wilayani kwake kuhakikisha wanaitunza miti iliyopandwa na itakayoendelea kupandwa katika maeneo mbalimbali ya makazi, maofisini, shuleni na pembezoni mwa barabara.

Mhe. Shimo ametoa rai hiyo Tarehe 08/12/2022 alipokuwa akizungumza na wanafunzi wa Shule ya msingi Mbugani aliposhiriki zoezi la upandaji miti katika shule hiyo ikiwa ni sehemu ya kuelekea kilele cha Maadhimisho ya Juma la Uhuru wa Tanzania Bara hapo tarehe 9 Disemba 2022.

Mkuu wa Wilaya ya Geita ameeleza kuwa kwa kupanda na kutunza miti ni sehemu ya utunzaji mazingira kadhalika zoezi la upandaji miti katika juma la Uhuru ni historia kwa vizazi vijavyo ambapo watakuwa wanakumbuka matukio yaliyofanyika wakati wa maadhimisho ya miaka 61 ya Uhuru katika Wilaya ya Geita kwa mwaka 2022.

Mhe. Shimo amewaeleza wananchi wa Wilaya ya Geita pamoja na watumishi wa taasisi mbalimbali za Serikali na binafsi kujenga desturi ya kupanda miti kwa wingi katika maeneo yao ili kupata faida za miti ikiwa ni pamoja na kuwapatia matunda, kivuli, mbao pia kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kurudisha uoto ulioharibiwa.

Kwa upande wake Kaimu Mhifadhi misitu Wilaya ya Geita Ndg. Sandusy C. Nguyale ameeleza kuwa katika Maadhimisho ya juma la miaka 61 ya Uhuru wa Tanzania Bara jumla ya miti 12,550 imepandwa katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Geita na ameendelea kuwahimiza wananchi na taasisi mbalimbali za Umma na binafsi Kwenda kuchukua miche ya miti katika kitalu cha Wakala wa Huduma za Misitu (TFS) kilichopo eneo la Usindakwe Kata ya Buhalahala Geita mjini na kupanda katika maeneo yao ili kufikia malengo ya kupanda miti 1,500,000 kwa mwaka 2022/2023.

Maadhimisho ya juma la Uhuru wa miaka 61 ya Tanzania Bara yanayoongozwa na kauli isemayo “Miaka 61 ya Uhuru Amani na umoja ni nguzo kwa Maendeleo yetu.” Wilayani Geita yamepambwa kwa shughuli mbalimbali zikiwemo usafi wa mazingira katika maeneo ya masoko, shuleni na kwenye makazi ya watu, upandaji miti, mashindano ya michezo mbalimbali kwa wanafunzi, midahalo na kutembelea shule ya wanafunzi wenye mahitaji maalum Mbugani pamoja na wafungwa katika gereza la Geita


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa