• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wananchi Geita Waaswa Kuendeleza Uzalendo

Posted on: December 10th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mheshimiwa Hashim Komba amewaasa wananchi wa Wilaya ya Geita kushiriki kuinua uchumi wa Nchi kwa kufanya kazi kwa bidii na kuwa wazalendo sambamba na kutafakari kwa kina ndani ya miaka 63 ya Uhuru wa Nchi ya Tanzania walipotoka, walipo sasa na wanapoelekea .

Mhe. Komba ameyazungumza hayo alipomwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela kwenye Kongamano la Wadau lililofanyika katika Ukumbi wa Gedeco Halmashauri ya Mji wa Geita wakati wa Maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara tarehe 9 Disemba 2024.

Mkuu wa Wilaya ya Geita ameeleza kuwa waasisi wa Nchi ya Tanzania walitumia uwezo wao na uzalendo wa hali ya juu kuifikisha Nchi ya Tanzania mahali ilipo hususan mafanikio katika sekta mbalimbali kama elimu, afya, maji, barabara na nyinginezo.

Akizungumza namna maisha yalivyokuwa kipindi Nchi ya Tanzania inapata uhuru, Mzee Samwel Majura ambaye ana umri wa miaka 75 ametoa rai kwa vijana wa sasa kuacha tabia ya kuibeza Serikali kuwa haijafanya lolote wakati katika kipindi cha nyuma wananchi walitembea umbali wa Zaidi ya kilomita 20 kufuata huduma za afya katika Hospitali moja tu iliyokuwa Geita mjini hali iliyopelekea baadhi ya kina mama kujifungulia njiani lakini ndani ya miaka 63 ya Uhuru Serikali imejenga zahanati kila kijiji na vituo vya afya vya kutosha.

Kwa upande wake Mzee James Zomola mwenyeji wa Wilaya ya Geita ambaye alianza elimu yake katika darasa maarufu kipindi hicho “Bush School” ameeleza kuwa wakati Nchi inapata uhuru kutoka kwa wakoloni shule zilikuwa chache sana na hakukuwa na walimu wa kutosha hali iliyosababisha wanafunzi wengi kushindwa kuendelea na masomo, kuchaguliwa kuendelea na elimu ya sekondari ilikuwa ni bahati sana lakini sasa hivi Serikali imejenga shule nzuri za sekondari kila kata na zenye walimu wa kutosha.

“ Mimi binafsi naweza kutoa ushuhuda wa Sekta ya maji kwa namna ambavyo ndani ya kipindi cha miaka 63 ya Uhuru imeboreshwa kwa kiwango kikubwa sana, wananchi wanapata huduma za maji majumbani kwao au jirani kabisa na maeneo wanayoishi tofauti na miaka ya nyuma ambapo maji yaliyotumika yalitokana na chemichemi, mito na maziwa. Nakumbuka kwa wakazi wa Kata ya Kasamwa ambao chanzo chetu cha maji ilikuwa ni chemichemi wakati wa kiangazi maji yalikuwa yanakauka na kulazimu watu wenye baiskeli tu kufuata maji Geita mjini katika kisima cha asili Lwenge.” Aliongeza Mzee James Zomola.

Maadhimisho ya miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara katika Mkoa wa Geita yaliyobebwa na kauli mbiu isemayo “Miaka 63 ya Uhuru wa Tanzania Bara: Uongozi madhubuti na ushirikishwaji wa wananchi ni msingi wa maendeleo yetu.” Kadhalika wananchi waliohudhuria katika Kongamano la Uhuru walipata kufahamu Historia ya harakati za kupata Uhuru wa Tanzania na mchango wa viongozi wa Taifa katika Maendeleo ya kiuchumi, Tanzania na harakati za mapinduzi ya kiuchumi katika sekta za elimu, afya, maendeleo ya jamii, kilimo, miundombinu, nishati, biashara, mawasiliano na ujenzi kupitia mada zilizowasilishwa na wataalam wa kada mbalimbali.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • MKUTANO MAALUMU WA BARAZA WA KUJADILI MAJIBU YA HOJA NA MAPENDEKEZO YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    June 11, 2025
  • BILIONI 19.1 KUTEKELEZA UJENZI KITUO KIKUU CHA MABASI MANISPAA YA GEITA

    June 06, 2025
  • WATUMISHI GEITA MANISPAA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI ZA UTUMISHI WA UMMA

    June 05, 2025
  • WATUMISHI WA MANISPAA YA GEITA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MITANDAO YA KIJAMII YENYE TAARIFA ZA UPOTOSHAJI

    June 04, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa