• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wanafunzi Wajipatia Vifaa Vya Usafi Kutoka Plan International

Posted on: August 12th, 2020

Wanafunzi  Wajipatia  Vifaa vya Usafi Kutoka Plan International

Jumla ya Shule 77 za Msingi na Sekondari katika Halmashauri ya Mji wa Geita na Wilaya ya Geita wamepatiwa vifaa vya usafi ambavyo ni sabuni,taulo za kike, vifaa vya kunawia mikono,vifaa vya shule kama madaftari na kalamu kutoka Shirika la Plan International Tanzania.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa zoezi hilo lililofanyika Tarehe 10/8/2020 katika viwanja vya Shule ya Msingi Nyanza Geita mjini Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amelishukuru shirika la Plan kwa kutoa vifaa vya usafi mashuleni ambavyo vitawasaidia wanafunzi kujikinga na maradhi mbalimbali kama magonjwa ya kuhara, kipindupindu, trakoma na magonjwa ya macho na ngozi.

Mhandisi Robert Gabriel ameongeza kuwa Serikali ya Mkoa wa Geita itaendelea kulienzi shirika la Plan kwa mazuri wanayoyatenda na kuyataka mashirika mengine kuiga mfano wa Shirika la Plan. Pia amelipongeza shirika hilo kwa kutoa elimu juu ya namna bora ya unawaji mikono kwa makundi mbalimbali kama watu wenye ulemavu, wahudumu wa afya ngazi ya jamii na   walimu 680 kutoka shule za Msingi na Sekondari katika Wilaya ya Geita.

“Nina Imani kuwa wananchi wa Geita kwa sehemu kubwa wamenuafaika kwa elimu iliyotolewa kwa makundi mbalimbali ambapo walifundishwa namna ya kunawa mikono kipindi nchi yetu ilipokuwa inajikinga na ugonjwa wa Corona. Pia napenda nitoe wito kwa wanafunzi wote mtakaonufaika na vifaa hivi vya usafi kusoma kwa bidi ili muweze kufanikiwa kwenye maisha yenu ya baadaye.” Aliongeza Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Kwa upande wake Meneja Mradi wa Mkoa wa Geita Ndg. Adolf Kaindoa amesema kuwa Shirika la Plan International limeona ni vyema kutoa vifaa vya usafi hasa sabuni za maji katika juhudi zake za kuhakikisha watoto wanalindwa na magonjwa ya mlipuko ambapo kila shule itapatiwa galoni 10 za sabuni ya maji.Kadhalika Shirika limetoa 62(Tippy-Taps) vya kunawia mikono kwa watu wenye ulemavu katika Mkoa wa Geita, vifaa ambavyo vitapelekwa kwenye vituo vya afya ili kulinda afya zao dhidi ya magonjwa yanayosababishwa na uchafu.

Ndugu Kaindoa ameahidi kuwa shirika lake litaendelea kushirikiana na Serikali katika kuweka mikakati zaidi ya kuhakikisha haki za msingi za watoto, changamoto mbalimbali zinazowakabili zinatafutiwa ufumbuzi. Pia kuhakikisha vitendo vya ukatili kwa watoto vinatokomezwa katika Mkoa wa Geita.

Akiongea kwa niaba ya walimu wa shule zilizonufaika Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana Nyankumbu Mwl. Georgia Mugashe amelishukuru  Shirika la Plan kwa huduma kubwa na ya mfano waliyoitoa hususani ugawaji wa taulo za kike kwa wanafunzi kwa sababu kuna baadhi ya mabinti wanapata changamoto kubwa shuleni wanapokuwa katika kipindi cha hedhi kwa kukosa vifaa vya uhakika vya kujisitiri.

Vifaa vya kunawia mikono,Taulo za wanafunzi wa kike, sabuni, madaftari na kalamu kwa shule 77 za msingi na sekondari pamoja na vituo vya afya katika Halmashauri mbili za Wilaya ya Geita vilivyotolewa na Shirika la Plan International Tanzania vimegharimu jumla ya Shilingi 63,960,000/= za kitanzania.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa