• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

WANAFUNZI WA KOZI YA AWALI YA JESHI LA AKIBA WAPATIWA ELIMU YA HABARI

Posted on: July 4th, 2025

Halmashauri ya Manispaa ya Geita kupitia Kitengo cha Mawasiliano Serikalini leo tarehe 04 Julai, 2025 kimetoa elimu ya Habari na Saikolojia kwa Wanafunzi wa kozi ya awali ya Jeshi la Akiba yanayoendelea katika Kata ya Kalangalala, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuwajengea uwezo wa kitaaluma na kisaikolojia ili kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi na weledi katika mazingira mbalimbali ya kijamii na kijeshi.

Akizungumza wakati wa utoaji wa elimu hiyo, Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ndg. Justine Mbilinyi amesema kuwa kwa hali ya sasa, askari anahitaji si tu ujuzi wa kijeshi, bali pia uelewa wa kina kuhusu Elimu ya Habari na kufahamu mienendo ya binadamu kupitia saikolojia ya msingi.

“Vyombo vya habari ni nguzo muhimu katika jamii yoyote inayolenga maendeleo ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kitamaduni hivyo elimu ya habari itawasaidia  kuelewa umuhimu wa mawasiliano sahihi, matumizi ya vyombo vya habari, na tahadhari dhidi ya taarifa za upotoshaji” alieleza Mbilinyi

Naye, Mpiga Picha wa Halmashauri ya Manispaa ya Geita, Ndg. Damasen Leonard akiwasilisha mada ya Saikolojia amesema,

"Elimu ya saikolojia inawapa uwezo wa kutambua hali za kiakili na kihisia za watu, hali inayosaidia kujenga uhusiano mzuri baina ya askari na jamii"

Ndg. Damasen ameongezea kusema, Askari wa Jeshi la Akiba ana nafasi kubwa katika kuleta utulivu, usalama na mshikamano wa kitaifa. Ili kutimiza wajibu huo kikamilifu, ni lazima awe na uelewa mzuri wa saikolojia ya watu na pia aweze kutofautisha kati ya jambo sahihi na lisilo sahihi katika utekelezaji wa majukumu yake. Nidhamu, weledi, uadilifu na huruma ni nguzo za mafanikio kwa askari yeyote anayetaka kulitumikia taifa kwa heshima.

  1. Katika mafunzo haya mada zilizofundishwa ni pamoja na:
  2. Historia ya vyombo vya habari kuanzia kipindi cha ukoloni hadi zama za kidijitali.
  3. Umuhimu wa vyombo vya habari wakati wa amani na wakati wa vita.
  4. Kufahamu namna ya kutoa na kupata habari kutoka kwa wananchi.
  5. Saikolojia ya watu na umuhimu wa kujua mambo yanayopaswa na yasiyopaswa kufanywa na askari wa jeshi la akiba.

Akizungumza kwa niaba ya Mshauri wa Jeshi la Akiba Wilaya ya Geita na wanafunzi, MT 82691 Drill SGT wa kozi Simon Lazaro Byejwe katika Wilaya ya Geita ambaye ni Msaidizi wa Mshauri wa Jeshi la akiba wamekishukuru Kitengo cha Mawasiliano kwa Elimu waliyoitoa na kufurahishwa na masomo hayo, akisema kuwa limewasaidia kujitambua, kujenga uwezo wa mawasiliano bora, na kupata maarifa yatakayowasaidia ndani na nje ya jeshi.


MATUKIO MBALIMBALI KATIKA PICHA






TUFUATILIE KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII
Instagram

Facebook

X

Youtube

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA KOZI YA AWALI YA JESHI LA AKIBA WAPATIWA ELIMU YA HABARI

    July 04, 2025
  • WATUMISHI WAKUMBUSHWA KUFANYA KAZI KWA UMOJA

    June 30, 2025
  • BONAZA LA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA

    June 28, 2025
  • WANANCHI WA MANISPAA YA GEITA WAKUMBUSHWA KUENDELEA KUFANYA USAFI

    June 28, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa