• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Walimu Watakiwa Kuimarisha Vipindi Vya Dini Mashuleni

Posted on: August 6th, 2021

Walimu Watakiwa Kuimarisha Vipindi Vya Dini Mashuleni

Walimu wa Shule zote za msingi na sekondari nchini wametakiwa kuimarisha ufundishaji wa somo la dini kwa wanafunzi ili Watoto hao wakue kiimani na kuwa na hofu ya Mungu itakayowawezesha kuishi mazingira yoyote katika misingi ya maadili mema.

Ushauri huo umetolewa na Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa ana Serikali za Mitaa Mhe. David Silinde wakati wa ziara yake alipotembelea utekelezaji wa miradi mbalimbali katika sekta ya elimu na barabara ndani ya Halmashauri ya Mji wa Geita hivi karibuni.

Mhe. Silinde alitoa wazo hilo baada ya kukagua miundombinu ya maabara, darasa na bweni moja la wanafunzi ambayo imeharibiwa kwa kuchomwa moto katika Shule ya Sekondari Geita kwa nyakati tatu tofauti na kutamka kuwa hatua kali za kinidhamu zitachukuliwa dhidi ya wanafunzi wote watakaobainika kushiriki katika matukio yote maovu na waliohusika katika uharibifu wa miundombinu inayojengwa kwa gharama kubwa na Serikali.

“Wazazi ndio kitovu kikuu cha malezi ya Watoto, tafadhali timizeni wajibu wenu katika kuhakikisha mnawalea Watoto wenu katika misingi inayokubalika ili kujenga taifa lenye maadili, Kadhalika walimu mnatakiwa kudhibiti nidhamu ya wanafunzi wenu wanapokuwa shule maana huo ni wajibu wenu kama walezi wa hawa wanafunzi.” Aliogeza Naibu Waziri Tamisemi.

Akikagua ujenzi wa madarasa ya kisasa katika Shule ya Msingi Ukombozi Mhe. Silinde ametoa pongezi kwa uongozi wa Shule hiyo na kata nzima ya Nyankumbu kwa ubunifu wa kutumia milioni 64 waliyopewa na Serikali kupitia mradi wa lipa kulingana na matokeo (EP4R) kujenga madarasa 5 na mashimo 13 ya vyoo badala ya madarasa 3 na mashimo 4 ya vyoo.

Naibu Waziri Tamisemi amempongeza Diwani wa Kata ya Buhalahala Mhe. Dotto Zanzui Ludeha kwa moyo wa majitoleo ya ardhi aliyoitoa bure kwa wananchi wa kata yake ambapo shule mpya ya msingi inajengwa kwa gharama ya shilingi milioni 250 za huduma za kampuni kwa jamii (CSR) kutoka Mgodi wa Dhahabu wa Geita. Mhe. Silinde aliwashukuru kampuni ya GGM kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati.

Miradi mingine iliyotembelewa na Naibu Waziri wa Tamisemi wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Mji Geita ni Pamoja na ujenzi wa barabara ya Mwanza junction hadi Sirro Barracks kwa kiwango cha lami, ujenzi wa barabara ya Upendo Dispesary- American chips kwa kiwango cha lami nyepesi, Maktaba ya wanafunzi na mabweni mawili mapya katika Shule ya Sekondari Geita Pamoja na ujenzi wa bwalo la chakula katika Shule ya Sekondari Mwatulole.




Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa