• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Fedha na Biashara
      • Mipango na Takwimu
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Mipango Miji
      • Maendeleo ya Jamii,Ustawi wa Jamii na Vijana
      • Ujenzi
      • Mazingira na Usafishaji
    • Vitengo
      • Uchaguzi
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Nyuki na Misitu
      • Sheria
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha

Walimu 668 Geita Mji Wanufaika na Vishikwambi

Posted on: January 18th, 2023

Walimu 668 Geita Mji Wanufaika na Vishikwambi

Jumla ya wataalam 668 kutoka Idara za Elimu msingi, Sekondari, Waratibu Elimu Kata pamoja na walimu wa shule zote za umma za Msingi na Sekondari katika Halmashauri ya Mji Geita wamegawiwa vishikwambi (Tablets) ambazo zilinunuliwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ajili ya zoezi la Sensa ya watu na Makazi mwaka 2022.

Akikabidhi vishikwambi hivyo kwa Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Tarehe 18/1/2023 wakati wa hafla fupi ya kuwakabidhi walimu iliyofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Halmashauri mtaa wa Magogo, Mthibiti ubora wa shule Halmashauri ya Mji Geita Bi. Violet Kiiza ameeleza kuwa baada ya zoezi la Sensa ya watu na Makazi kukamilika Serikali iliazimia kuvigawa kwa sekta ya elimu kwa lengo la kuboresha utendaji kazi za kila siku na kuleta ufanisi kwenye taaluma.

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita Ndugu Egidy Teulas amewaasa walimu waliopewa vishikwambi hivyo kuvitumia kwa ajili ya kutunza kumbukumbu za taaluma shuleni, utunzaji wa takwimu sahihi za idadi ya wanafunzi, miundombinu ya shule pamoja na kuperuzi taarifa mbalimbali zitakazowezesha kuboresha taaluma ya wanafunzi.

“ Sitarajii mwalimu hata mmoja ambaye amepatiwa kishikwambi leo baada ya siku kadhaa nipate taarifa anakitumia katika matukio mbalimbali ya kihalifu yanayoendelea kwenye jamii au Kwenda nacho sehemu za starehe na kuvitelekeza huko, bali mnatakiwa mhakikishe mnatunza mali za Serikali ili viweze kudumu na kuwanufaisha walengwa.” Aliongeza Ndg. Egidy Teulas.

Wakitoa neno la shukrani kwa niaba ya walimu wote Bw. Brighton Samuel Mratibu Elimu kata ya Kasamwa na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kivukoni Ndg. Ndatu Said Maduka wameipongeza Serikali ya awamu ya sita chini ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwachagua walimu kupatiwa vishikwambi hivyo miongoni mwa watumishi wote wa umma katika kada mbalimbali.

 Walimu hao wameahidi kutovitumia vishikwambi hivyo katika matukio ambayo ni kinyume cha sheria na taratibu za utumishi wa umma bali vitatumika  kwa matumizi yaliyokusudiwa ikiwemo  kupata taarifa muhimu za kitaaluma kwa haraka na manufaa yake yataonekana baada ya kipindi kifupi kwani kazi zao zitaboreshwa Zaidi kupitia vitendea kazi hivyo.



Matangazo

  • TANGAZO LA URASIMISHAJI WA MAKAZI YASIYOPANGWA January 16, 2023
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI July 22, 2022
  • TANGAZO LA KAZI ZA MACHINJIO August 16, 2022
  • MATOKEO YA MTIHANI WA DARASA LA SABA GEITA MJI December 02, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • Kamati Ya Siasa Wilaya Ya Geita Yaridhishwa na Miradi Geita Mji

    January 26, 2023
  • Walimu 668 Geita Mji Wanufaika na Vishikwambi

    January 18, 2023
  • Wanufaika Washauriwa Kuanzisha Viwanda Vidogo

    December 27, 2022
  • Timu Ya Halmashauri Yapata Udhamini Kutoka GGM

    December 20, 2022
  • Zaidi

Video

Machinjio ya Kisasa Mpomvu Yaanza kazi
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Applications Forms
  • Acts
  • Barua pepe za watumishi
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa