• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wakulima Washauriwa Kulima Pamba Kibiashara

Posted on: August 29th, 2017

Wakulima Washauriwa Kulima Pamba Kibiashara


Wakulima wilayani Geita wameshauriwa kubadilisha mfumo wa kilimo cha pamba ili kuinua kilimo hicho na kufanya kiwe kilimo cha biashara kama ilivyo kwa mazao mengine.


Ushauri huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Geita Ndg. Herman Kapufi wakati wa Kikao na Maafisa Ugani, Watendaji wa Kata na Wataalam wa Kilimo kutoka kata zote za Halmashauri ya Mji Geita na Halmashauri ya Wilaya, kilichofanyika Tarehe 23/8/2017 katika Ukumbi wa Halmashauri ya Mji Geita.


Mkuu wa Wilaya ya Geita amewaagiza Maafisa Ugani na Wataalamu wa Kilimo kutoka Halmashauri hizo kuhakikisha kuwa katika msimu wa kilimo unaotarajia kuanza kilimo cha mkataba kitiliwe mkazo ili kupata matokeo makubwa ya zao la pamba na kuongeza mapato ya Halmashauri na pato la Taifa kwa ujumla.


Amefafanua kuwa baadhi ya mikakati ambayo itafanikisha kilimo cha pamba chenye tija ni pamoja na Kutumia kilimo cha mkataba , Maafisa ugani wawezeshwe kupata usafiri utakaowasaidia kusafiri umbali mrefu kufuatilia mashamba ya pamba, Wakulima wahamasishwe kutokwepa kulima pamba katika maeneo yote na kuainisha mahitaji muhimu katika kilimo cha pamba.


Kwa upande wake Mshauri wa mfumo wa kilimo cha Mkataba kutoka Taasisi ya Gasp Afica Ndg. Joshua Mirumbe amesema kuwa tafiti zinaonyesha kuwa uzalishaji wa zao la pamba umeshuka kutoka kilo milioni 40 miaka 7 iliyopita hadi kilo milioni 12 kwa sasa katika Mkoa wa Geita, hali hii imepelekea viwanda vya kuchambua pamba vilivyoko nchini kukosa malighafi ya kufanyia kazi.


Ndg. Mirumbe amaeongeza kuwa Maafisa ugani wanatakiwa waunge mkono juhudi za Serikali katika kuhamasisha mfumo wa kilimo cha mkataba kwa sababu wakijipanga vyema ni mfumo ambao utaleta matokeo chanya ya uzalishaji. Pia unaipa nguvu Serikali kusimamia vyema kwa sababu Kampuni itakayohitaji kufanya kazi na wakulima kutambulisha utaratibu wa huduma zake na kushirikiana na Halmashauri husika  katika utekelezaji.


“Watendaji wa kata zote mnatakiwa kuwa wasimamizi wakuu kwa kujua shughuli zote jinsi zitakavyofanyika katika maeneo yenu pindi utekelezaji utakapoanza. Pia msihusishe na  kilimo cha pamba kilichokuwa kikisimamiwa na Umoja wa Wachambuzi wa Pamba( UMWAPA) ambacho hakikufanikiwa kwa sababu sekta binafsi ziliruhusiwa kufanya kazi moja kwa moja na mkulima pasipo usimamizi wa Serikali.” Aliongeza Ndg. Mirumbe.


Akizungumza kwa niaba ya wataalamu wa kilimo Ndg. Daniel Kulunguja ametoa ushauri wa kuwa na kampuni Zaidi ya moja itakayotumika kugawa pembejeo za kilimo cha zao la Pamba  ili kuleta ushindani wa kibiashara na ufanisi wa Kilimo cha mkataba.


Mfumo wa Kilimo cha Mkataba kwa zao la pamba ni utaratibu uliowekwa na Serikali ambapo Kampuni za Uchambuzi wa Pamba hutoa kwa mkopo  mbegu, dawa za kunyunyiza, mabomba ya kunyunyizia dawa  kwa wakulima wa zao la pamba katika maeneo mbalimbali ya nchi ya Tanzania ambako zao la pamba linalimwa na marejesho ya mkopo huo hufanyika baada ya wakulima hao kuvuna pamba zao.





Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa