• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wakulima Wahimizwa Kulima Kwa Tija

Posted on: October 5th, 2021

Wakulima Wahimizwa Kulima Kwa Tija

Wakulima katika Wilaya ya Geita wamehamasishwa kulima kisasa na kitaalam Zaidi ili kuboresha Maisha yao binafsi, jamii nzima na kuongeza pato la Taifa litokanalo na kilimo.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Geita Mheshimiwa Wilson Shimo wakati wa ziara yake ya kikazi katika Tarafa za Kasamwa na Geita kwa lengo la kuzungumza na wakulima hususan wa zao la pamba kabla ya kuanza msimu wa kilimo hivi karibuni

Mhe. Shimo ameongeza kuwa ni dhahiri  kila mtanzania anatambua mchango wa maendeleo ya kilimo katika nchi hii, uzalishaji wa mazao bado si wa kuridhisha sana hivyo ni jukumu lake kama kiongozi kushauri na kuwakumbusha wakulima wa zao la pamba na mazao mengine kuzalisha kwa kuzingatia kanuni bora za kilimo ili kuwa na kilimo chenye tija.

Mkuu wa Wilaya ya Geita amewataka mawakala wa pembejeo za kilimo kuwasilisha mahitaji yote kwa wakulima kabla ya msimu wa kilimo kuanza na kuwatahadharisha wakulima kuepuka tabia za uvivu, kesi zisizo na msingi, kuzurula hovyo katika msimu wa kilimo badala yake wajitahidi kuendana na ratiba za kilimo

“Natoa agizo kwa vyama vote vya msingi vya kilimo na ushirika (AMCOS) kulima shamba la ekari tano kwa kila chama katika msimu unaoanza karibuni Kadhalika maafisa ugani katika kata zote wahakikishe hawakai maofisini bali wanatoka kwenda mashambani kuwasaidia wakulima na wao pia wanatakiwa kuanzisha mashamba darasa ya mfano katika kila kata ili wakulima wajifunze kwa vitendo”. Aliongeza Mhe. Shimo

Kwa upande wa mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita Afisa Kilimo, Ushirika na Umwagiliaji Bw. Leonard Chacha amewaahidi wakulima kuwa yeye na maafisa ugani wake watashirikiana kuhakikisha changamoto zote zitakazojitokeza kwenye mashamba yao zinapatiwa ufumbuzi kwa muda muafaka.

Mkaguzi wa Pamba kutoka Bodi ya Pamba Tanzania Pamoja na wataalam wa ugani wa Halmashauri ya Mji Geita wametoa elimu ya vitendo juu ya kanuni kumi za kilimo bora cha pamba baadhi ni Pamoja na kutumia mbolea za samadi na virutubisho vingine, kupanda pamba mapema, kupanda kwa mistari na nafasi maalum, kupanda idadi halisi ya mbegu katika kila shimo, kupalilia kwa wakati , kunyunyiza madawa kuzuia wadudu waharibifu na kuvuna pamba mapema.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa