• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wajumbe wa ALAT Wapongeza Miradi Halmashauri ya Mji Geita

Posted on: July 1st, 2019

Wajumbe ALAT Wapongeza Miradi ya Mji Geita

Wajumbe wa Jumuiya ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa( ALAT) Mkoa wa Geita wamepongeza juhudi zinazofanywa na Halmashauri ya Mji wa Geita katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Maendeleo yenye kiwango cha hali ya juu.

Pongezi hizo zimetolewa wakati wa ziara waliyoifanya wajumbe hao hivi karibuni katika Halmashauri ya Mji Geita ambapo walitembelea miradi ya ujenzi wa Soko kuu Geita mjini, Barabara ya lami Madini- Bomani- KKKT, Kikundi cha vijana kinachojishughulisha na ufugaji kuku katika mtaa wa Katoma na Ujenzi wa Ofisi ya Kata ya Bombambili.

Akizungumza walipotembelea ujenzi wa Ofisi ya Kata ya Bombambili, Mwenyekiti wa ALAT Mkoa wa Geita Mhe. Elisha Lupuga amemsifu Diwani wa Kata ya Bombambili pamoja na watumishi wake pamoja na Menejimenti nzima ya Hlmashauri ya Mji wa Geita kwa ujenzi huo wa Ofisi nadhifu na kuahidi kuchangia Shilingi 2,000,000/= kutoka mfuko wa ALAT kwa ajili ya ujenzi wa mradi huo.

Afisa Tawala msaidizi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita Bi. Sania Mwangakala pamoja na pongezi alizozitoa kwa Halmashauri ya Mji wa Geita amewataka wajumbe kutoka kwenye Halmashauri nyingine ndani ya Mkoa wa Geita waige mfano kwa kujenga ofisi za mitaa, vijiji na Kata katika maeneo yao ili watumishi walioko katika maeneo hayo wapate mazingira rafiki ya kufanyia kazi.

Akizungumza katika mtaa wa Katoma walipotembelea kikundi cha Penye nia ambacho kinajishughulisha na ufugaji kuku wa kisasa ambacho kimekopeshwa Shilingi 5,000,000/=kutoka katika asilimia tano ya Mapato ya ndani ya Halmashauri na chenye wanachama watano, Mhe. Safari Mayala, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe amewashauri wanachama kutafuta eneo kubwa kwa ajili ya ufugaji kuku utakaowapatia faida zaidi kuliko eneo walilonalo hivi sasa.

Timu ya Wajumbe wa ALAT Mkoa wa Geita wamefanya ziara hiyo katika Halmashauri ya Mji wa Geita ikiwa ni sehemu ya kikao chao cha robo ya tatu ambapo hufanya vikao vyao kila robo ya Mwaka wa fedha katika Halmashauri za Mkoa wa Geita kulingana na ratiba ya mzunguko waliopanga.




Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa