• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wahandisi Wahimizwa Kutimiza Wajibu

Posted on: January 30th, 2024

Wahandisi Wahimizwa Kutimiza Wajibu 

Wahandisi katika Halmashauri ya Mji Geita wamekumbushwa kutimiza wajibu wao kwa kusimamia ujenzi wa miradi kikamilifu ili kuwa na majengo imara na yenye ubora ambayo yatawanufaisha wananchi katika maeneo yao.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Geita walipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo iliyotekelezwa katika kipindi cha miezi sita kuanzia mwezi Julai hadi Disemba 2023.

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Geita Ndugu Barnabas Mapande ametoa pongezi za dhati kwa Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha nyingi kwa Halmashauri ya Mji Geita kwa ajili ya ujenzi wa miradi mbalimbali ya maendeleo.

Ndg. Barnabas Mapande amewapongeza wananchi wa mtaa wa Mwilima Kata ya Kanyala na Mbunge wa jimbo la Geita mjini kwa kuanzisha mradi wa Zahanati ili kuondoa kero ya  wagonjwa hususan wanawake wajawazito na Watoto wanaotembea umbali mrefu kufuata huduma za matibabu katika Kituo cha Afya Kasamwa.

“Mwishoni mwa mwaka 2025 mradi mkubwa wa maji unaotekelezwa katika miji 28 Tanzania utakamilika na kuifanya Geita kujivunia mafanikio ya kupata maji mengi ikiwa ni mojawapo ya jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha watanzania wanapata huduma ya uhakika ya maji safi na salama.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Cornel Magembe ameahidi kushirikiana na Mamlaka ya Maji safi Mjini Geita kusimamia mradi huo na kuhakikisha unakamilika ndani ya muda uliopangwa ili wananchi wa Wilaya ya Geita waweze kuondokana na kero ya upungufu wa maji unaopelekea maji kutoka kwa zamu.

Wakiwa katika ukaguzi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya wasichana Geita wajumbe wa Kamati ya Siasa wamempongeza Diwani wa Kata ya Bombambili inapojengwa shule hiyo Mhe. Leonard Bugomola kwa namna anavyojitoa kutatua changamoto mbalimbali na kuhakikisha miradi katika Kata yake inatekelezwa kwa kiwango cha hali ya juu.

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Wilaya ya Geita Bi. Paulina Majogoro amesema kuwa Shule ya Sekondari ya wasichana Geita itawakomboa Watoto wa kike ambao Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekusudia kuwawezesha kutimiza ndoto zao kupitia fursa ya elimu bila malipo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa wafanyabiashara kata ya Kasamwa Bw. Faustine Kitula ameeleza kuwa ujenzi wa Barabara ya lami kwa kiwango cha lami nyepesi kilomita 0.5 Kasamwa senta utakapokamilika wataepukana na vumbi katika maduka na biashara zao zilizoko pembezoni mwa Barabara hiyo.

Miradi iliyotembelewa na wajumbe wa Kamati ya Siasa ya Halmashauri kuu ya CCM Wilaya ya Geita ni ujenzi wa Shule ya SekondariNyantoroto, ujenzi wa Shule ya Sekondari ya kitaifa ya wasichana Geita, mradi mkubwa wa maji, kutembelea kikundi cha vijana wanaojishughulisha na uuzaji wa viatu vua mitumba ambacho kimenufaika na mkopo uliotolewa na Halmashauri, ujenzi wa Zahanati ya Mwilima pamoja na ujenzi wa Barabara kwa kiwango cha lami nyepesi Kasamwa senta.






Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa