• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Wadau Wapongezwa Kwa Kuchangia Miradi Ya Maendeleo

Posted on: January 11th, 2024

Wadau Wapongezwa Kwa Kuchangia Miradi Ya Maendeleo

Serikali Mkoani Geita imeahidi kuendelea kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ambao wanajitoa kuunga mkono jitihada za Serikali ya awamu ya sita katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Geita Mheshimiwa Cornel Magembe alipokuwa akiongea na hadhara ya watu waliojitokeza kushuhudia makabidhiano ya vyumba saba vya madarasa na ofisi mbili za walimu katika Shule ya Msingi Nyamalembo ambavyo vimefanyiwa ukarabati na kampuni ya Usafirishaji Blue Coast Investment yenye makao makuu mjini Geita.

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Cornel Magembe ametoa pongezi za dhati kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Blue Coast Ndugu Ignas Athanas kwa namna kampuni yake ilivyojitoa katika kuhakikisha mazingira ya ujifunzaji na ufundishaji katika Shule ya msingi Nyamalembo yanaboreshwa na kuwaalika wadau wengine wa maendeleo kuiga mfano kutoka katika kampuni hiyo.

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya madarasa hayo, Mkurugenzi wa Kampuni ya Blue Coast ambaye pia ni mlezi wa Shule ya msingi Nyamalembo ameeleza kuwa baada ya kukabidhi chumba kimoja cha darasa chenye samani zote ndani yake mwishoni mwa mwezi Juni 2023 wananchi wa Kata ya Mtakuja wakiongozwa na Diwani wao Mhe. Costantine Morandi Mtani walimuomba awasaidie kukarabati madarasa chakavu shuleni hapo, suala ambalo alilipokea kwa mikono miwili na kufanikiwa kulitekeleza ndani ya kipindi kifupi.

Diwani wa Kata ya Mtakuja ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Geita Mhe. Costantine Morandi ametoa shukrani kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Blue Coast kwa kazi kubwa aliyoifanya katika Shule ya msingi Nyamalembo, ni Fahari kubwa kwao na pia ni ishara ya mahusiano mazuri yaliyopo baina ya Kampuni hiyo na jamii inayowazunguka. Mhe. Morandi ameahidi kwa niaba ya wananchi wake kuwa watayatunza kikamilifu madarasa hayo ili yaendelee kuvutia na kuwanufaisha wanafunzi.

Kwa upande wake Mwalimu mkuu wa Shule ya Msingi Nyamalembo Ndugu Josiah Mwombeki ameeleza kuwa ukarabati wa madarasa saba uliofanywa na Kampuni ya Blue Coast umewezesha kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia ambapo wanafunzi watajifunza wakiwa katika mazingira safi na salama, kupunguza utoro kwa wanafunzi kwani kutawafanya wapende kuhudhuria shuleni na kumaliza uhaba wa madarasa 12 uliokuwepo ambapo kwa sasa madarasa na samani ni toshelevu kwa wanafunzi wote.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa