• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Waathirika Wa Mvua Wametakiwa Kutunza Misaada

Posted on: December 6th, 2023

Waathirika wa Mvua Wametakiwa Kutunza Misaada

Mkuu wa Wilaya ya Geita Mheshimiwa Cornel Magembe amewaasa wananchi wa Kata za Kasamwa, Kanyala, Shiloleli na Bulela ambao nyumba zao ziliathiriwa na mvua kubwa zilizonyesha zikiambatana na upepo kuanzia Oktoba 18 hadi Novemba 10, 2023 kuhakikisha misaada waliyopatiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na wahisani wengine watakaojitolea inatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Mhe Magembe ameyasema hayo hivi karibuni alipokuwa akigawa msaada kwa waathirika hao kutoka Tarafa ya Kasamwa, shughuli ambayo ilifanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Kata ya Kasamwa ambapo amewataka waathirika wa mvua hizo kutumia vyema misaada hiyo na kuwaelekeza watendaji kufuatilia ili kuhakikisha misaada iliyotolewa haiuzwi wala kutumika kinyume na malengo.

Akiwasilisha taarifa ya maafa mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mratibu wa maafa Halmashauri ya Mji Geita Bi. Valeria Makonda amesema kuwa takribani nyumba 556 za makazi ya watu katika tarafa ya Kasamwa zimepata madhara yakiwemo kubomoka kabisa, kuezuliwa mapaa na kupata mipasuko.

Bi. Makonda ameeleza kuwa Halmashauri ya Mji imepokea vifaa vya msaada wa kibinadamu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Idara ya Menejimenti ya maafa. Vifaa vilivyotolewa ni pamoja na mahindi tani 22.1, magodoro 71, mablanketi 148, mikeka 148, ndoo 74 madumu 74 na vyombo seti 40.

Mratibu wa Maafa Geita Mji ameongeza kuwa tofauti na makazi ya watu mvua hizo zimeathiri Taasisi mbalimbali ambazo ni madarasa 28 ya shule za Msingi na Sekondari, nyumba mbili za walimu, Zahanati moja, Kituo kimoja cha afya, Ofisi moja ya Serikali ya mtaa, makanisa 9 na msikiti 1 ambapo kutokana na tathimini iliyofanyika katika majengo na taasisi za umma jumla ya shilingi 225,461,080 zinahitajika ili kukarabati na kujenga miundombinu iliyoathirika.

Kamati za maafa za Kata kwa kushirikiana na Kamati ya maafa ya Halmashauri wameendelea kutoa elimu juu ya kuhama katika maeneo ya mabonde ambayo ni hatarishi katika kipindi cha mvua. Pia wananchi wameendelea kushauriwa kutotumia au kubomoa kabisa majengo ambayo ni hatarishi ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza. Aidha wameendelea kushauriwa kutekeleza kampeni ya ujenzi wa nyumba bora kwa kutumia tofali za kuchoma au tofali mfungamano ambazo ni gharama nafuu.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • MKUTANO MAALUMU WA BARAZA WA KUJADILI MAJIBU YA HOJA NA MAPENDEKEZO YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    June 11, 2025
  • BILIONI 19.1 KUTEKELEZA UJENZI KITUO KIKUU CHA MABASI MANISPAA YA GEITA

    June 06, 2025
  • WATUMISHI GEITA MANISPAA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI ZA UTUMISHI WA UMMA

    June 05, 2025
  • WATUMISHI WA MANISPAA YA GEITA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MITANDAO YA KIJAMII YENYE TAARIFA ZA UPOTOSHAJI

    June 04, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa