• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Viongozi watakiwa kutunza usafi wa Mazingira

Posted on: July 25th, 2018

Viongozi Watakiwa Kutunza Usafi wa  Mazingira

Viongozi wa Serikali kuanzia ngazi ya Vitongoji wameagizwa kuonyesha jitihada za dhati katika kujituma kwa kushirikiana na wananchi wanaowaongoza kutunza usafi wa mazingira katika maeneo yanayowazunguka.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita  Mhandisi Robert Gabriel aliposhiriki katika zoezi la usafi wa mazingira katika Hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Geita na maeneo mbalimbali ya mitaa ndani ya Halmashauri ya Mji wa Geita pamoja na vijana wanaoshiriki mafunzo ya jeshi la akiba katika Wilaya ya Geita tarehe 25/07/2018, ikiwa ni siku ya kuwaenzi mashujaa wa Taifa la Tanzania waliotangulia mbele ya haki.

Kwa upande wake Mshauri wa jeshi la akiba katika Mkoa wa Geita, Luteni Kanali Daniel Mwadekela Mhagama amesema kuwa ni desturi ya majeshi ya ulinzi tarehe 25 Julai kila mwaka  kuwaenzi mashujaa ambao wametangulia mbele ya haki katika harakati za kuikomboa nchi ya Tanzania wakiwemo wale walioshiriki vita vya Kagera ambao wamezikwa eneo la Kaboya mkoani Kagera. Pia mashujaa waliopambana kupinga ukoloni akiwemo Chifu Mkwawa, Mirambo na wengineo.

“ Tumeamua kuwaenzi mashujaa wetu kwa kufanya usafi katika mitaa mbalimbali ya Halmashauri ya Mji wa Geita ili kuungana na wenzetu ambao wako jirani na makaburi ya kaboya na nalilendele, Mtwara ambao siku ya leo wanafanya usafi katika makaburi hayo .” Aliongeza Luteni Kanali Mhagama.

Mshauri wa Jeshi la akiba katika Mkoa wa Geita amesema kuwa licha ya majukumu mengi yanayotekelezwa na Jeshi la Wananchi, jeshi hilo linafanya kazi ya kufufua uzalendo hususan kwa kuwafundisha vijana wa jeshi la akiba ili watambue kwamba kazi ya kulinda Mkoa wa Geita na nchi nzima kwa ujumla ni shughuli ya kujitolea.

Mkuu wa Idara ya usafishaji na mazingira katika Halmashauri ya Mji wa Geita Ndg. Fredrick Linga amesema kuwa hali ya usafi katika mji wa Geita sio ya kuridhisha sana kwa sababu wananchi bado wanatupa taka hovyo barabarani. Hivyo ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kutiririsha maji machafu barabarani na kushiriki katika shughuli ya usafi wa mazingira kila jumamosi ya mwisho wa mwezi katika nyumba zao, mazingira yao ya kazi na mji mzima kwa ujumla.




Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa