• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

UZINDUZI WA MIRADI YA UJENZI

Posted on: November 17th, 2017

Halmashauri ya Mji Geita yazindua kampeni ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa na zahanati

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ameshiriki uchimbaji msingi wa nyumba ya walimu katika shule ya Msingi Shinamwendwa, ujenzi wa Shule ya Sekondari Mgusu na ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Nyakato katika Halmashauri ya Mji Geita.

Akizindua miradi hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Geita amepongeza jitihada inazofanywa na wananchi kwa kutambua raslimali za asili zinazopatikana katika maeneo yao na kuzitumia. Pia kushiriki katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo licha ya kuwepo changamoto mbalimbali zinazowakabili katika maisha yao.

Amesema kuwa viongozi wa Serikali kuanzia ngazi ya vitongoji hadi wilaya wawatie moyo wananchi hao na kutunza heshima ya dhamana ya uongozi waliyopewa katika jamii kwa kushirikiana na kusimamia kikamilifu utekelezaji wa miradi ya ujenzi iliyoanzishwa ambayo imeibuliwa na wanachi wa maeneo mbalimbali katika Halmashauri ya Mji wa Geita.

“ Wananchi wana kiu ya maendeleo na watu mtakaotimiza malengo yao ni viongozi hivyo mjitahidi kuwa waadilifu na wachapakazi ili kuwaridhisha wananchi na Serikali yao, kama namna Serikali ya awamu ya tano inavyounga mkono jitihada za wananchi wake”.Aliongeza Mkuu wa Mkoa.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Geita Ndg. Herman Kapufi amesema kuwa kuna baadhi ya wananchi ambao bado wana mtazamo wa kujengewa majengo yote na kutimiziwa mahitaji muhimu na Serikali pekee pasipo kuchangia chochote, hivyo mwananchi yeyote atakayekaidi kuchangia au kujitolea nguvu kazi katika shughuli za ujenzi aripotiwe katika ofisi yake na kuchukuliwa hatua madhubuti.

Mkuu wa Mkoa wa Geita alikuwa katika ziara ya kikazi yenye lengo la kuibua miradi ya majengo ya shule na zahanati ili kutimiza malengo ya kuwa na zahanati kwa kila kijiji kufikia mwaka 2020 na kujitahidi kupunguza uhaba wa vyumba vya madarasa katika Mkoa wa Geita ambapo mahitaji ni vyumba 8600 na vilivyopo sasa ni vyumba 571.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa