• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Tunzeni Vitabu Viwatunze - RC Shigela

Posted on: August 31st, 2022

Tunzeni Vitabu Viwatunze – RC Shigela

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mheshimiwa Martine Shigela amewaasa walimu na wanafunzi wilayani Geita kuhakikisha wanavitunza na kutumia kwa malengo vitabu vya sayansi ili viweze kuwasaidia watoto ambao watapata ujuzi utakaozalisha wanasayansi watakaoliwezesha Taifa kupiga hatua Zaidi katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia.

Mhe. Shigela ametoa kauli hiyo hivi karibuni alipokuwa akipokea jumla ya vitabu 52,683 vya masomo ya Hisabati, sayansi, Kiswahili na kingereza kwa shule 87 za msingi kuanzia darasa la nne hadi saba na vitabu vya kusoma, kuandika na kuhesabu kwa darasa la kwanza na pili, vifaa vya michezo na kujifunzia kwa watoto wenye ulemavu ambavyo vimetolewa na Shirika la Plan International, ambapo vitabu 43,800 kati ya hivyo vimenunuliwa kupitia mradi wa kuwawezesha wasichana kuendelea na masomo kwa kifupi KAGIS( Keeping Adolescent Girls in School) kwa ufadhili wa nchi ya Canada

Mkuu wa Mkoa wa Geita amelishukuru Shirika la Plan International kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika  kuwathamini wanafunzi na watoto wa Geita  kama ambavyo imezoeleka jamii kubwa ya kanda ya ziwa haitoi kipaumbele cha kumpatia elimu mtoto wa kike.

“Nawaagiza walimu wote ambao mmekabidhiwa vitabu muhakikishe mnatengeneza maktaba nzuri na zenye ubora ambazo mtazitumia kutunza vitabu hivyo ambavyo vitatumika kufundishia na wanafunzi watawekewa utaratibu maalum utakaowawezesha kusoma pasipo kufanya uharibifu kama kuchana kurasa za ndani na uharibifu mwingine”. Aliongeza RC Shigela.

Akishukuru kwa niaba ya uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Geita Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita Ndg. Egidy Teulas amesema kuwa ni vigumu kutaja maendeleo ya wilaya ya Geita pasipo kuwataja Plan Internationl kutokana na mchango mkubwa ambao wanatoa kwa jamii hususan katika masuala ya haki za watoto. Pia ameahidi kushirikiana na walimu wake kuvitunza vitabu walivyopewa ili view na manufaa kwa watoto ambao ni Taifa la kesho.

Kwa upande wake Meneja wa mradi wa KAGIS Ndg. Nicodemus Gachu ameeleza kuwa shirika la Plan International linatambua changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya elimu kama upungufu wa vitabu, nyumba za walimu hivyo wakaona ni vizuri wakaisaidia Serikali katika kupunguza mzigo mkubwa wa mahitaji kwa kutoa vitabu hivyo ambavyo vimenunuliwa kwa Zaidi ya shilingi milioni 438 za kitanzania.

Ndg. Gachu ameeleza kuwa kupitia mradi wa KAGIS jumla ya vyoo 50 vitajengwa katika shule za mradi kwenye mikoa ya Geita na Kigoma. Kadhalika kwa kipindi cha miaka mitano mradi utanunua na kusambaza jumla ya baiskeli 2200 kwa watoto wa kike wanaolazimika kutembea umbali mrefu kwenda shuleni pamoja na kutoa mafunzo juu ya afya ya uzazi na usawa wa kijinsia.

Mradi wa KAGIS ambao unatekelezwa katika mikoa ya Geita na Kigoma kwa miaka mitano umelenga kushughulikia changamoto zinazozuia wasichana walio katika umri balehe kutambua haki yao ya elimu salama, bora na inayozingatia jinsia pamoja na hayo mradi unachangia kutimiza malengo ya wizara ya elimu, sayansi na teknolojia katika kuhakikisha upatikanaji sawa na kukamilika kwa elimu ya msingi kwa wote.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa