• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

TUMIENI HEKIMA KUTUNZA MAZINGIRA-DC

Posted on: June 6th, 2018

TUMIENI HEKIMA KUTUNZA MAZINGIRA- DC

Wakazi wa Wilaya ya Geita wametakiwa kutumia busara na hekima  katika utunzaji wa mazingira katika  shughuli mbalimbali za kiuchumi na  kijamii wanazozifanya.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Geita Ndg. Herman Kapufi wakati akihutubia hadhara iliyoshiriki maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani yaliyofanyika kiwilaya katika kata ya Mgusu, Halmashauri ya Mji wa Geita tarehe 5/06/2018.

Ndg. Herman Kapufi amewasihi wananchi kuwa na nidhamu ya kufuata maelekezo yanayotolewa na wataalam wa mazingira kwa kuacha tabia ya kukata miti hovyo, kutunza vyanzo vya maji, kutotupa taka hovyo na kutumia nishati mbadala ya gesi na mkaa unaotumia mapumba badala ya mkaa wa miti unaotumika kwa wingi hivi sasa.

Mkuu wa Wilaya ya Geita ameongeza kuwa waharibifu wa Mazingira waonywe ili waache tabia ya kuharibu mazingira kiholela . Pia kila kaya ihakikishe inapanda miti ya aina mbalimbali kama ya matunda , kivuli na mbao ili kukabiliana na uchafuzi wa hali ya hewa.

Akizungumzia baadhi ya mikakati iliyowekwa na Wilaya ya Geita, Ndg. Kapufi amesema kuwa uongozi wa Wilaya ya Geita umedhamiria kufanya doria za mara kwa mara katika hifadhi za misitu, kutoa elimu kwa jamii iliyopakana na hifadhi, kugawa mbegu na miche ya miti ili kuweza kutunza mazingira, kuwafukuza wachimbaji wadogo wa dhahabu wanaochimba ndani ya hifadhi ya misitu.

Maafisa Mazingira na usafishaji wa Halmashauri za Wilaya ya Geita na Geita Mji wamebainisha changamoto zinazoukabili mji wa Geita kuwa ni wimbi kubwa la uharibifu wa mazingira kupitia uvunaji miti kwa ajili ya nishati, madini, kilimo, malisho ya mifugo na makazi, tatizo la utupaji taka ngumu ovyo ambapo asilimia kubwa ya taka  ina mifuko ya plastiki. Pia mabadiliko ya tabia nchi ambayo yanasababishwa na ukataji na uharibifu wa misitu.

Afisa Mazingira na Usafishaji wa Halmashauri ya Mji Geita Ndg. Pancrace Shwekelela amesema katika kukabiliana na changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi, jumla ya miti2, 157,535 imepandwa katika maeneo mbalimbali wilayani Geita. Ameongeza kuwa Idara ya Mazingira na udhibiti wa taka ngumu imekuwa ikisimamia shughuli za usafi wa Mazingira kwenye maeneo ya Umma kama mashuleni,kwenye masoko na maeneo ya wachimbaji wa dhahabu.

Siku ya Mazingira Duniani huadhimishwa  tarehe 5 Juni kila mwaka kwa lengo la kuhimiza jamii kutunza, kuhifadhi na kulinda mazingira na pia kuepuka athari zinazotokana na uharibifu wa Mazingira. Ujumbe wa siku hiyo kwa Mwaka huu ni “MKAA NI GHARAMA: TUMIA NISHATI MBADALA.”



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa