• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Teknolojia ya Tofali Fungamano kupunguza Uhaba wa Madarasa

Posted on: February 11th, 2020

Teknolojia ya Tofali Fungamano kupunguza Uhaba wa Madarasa

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ameziagiza Halmashauri zote katika Wilaya ya Geita kuhakikisha wanatumia matofali fungamano( Interblocking) katika ujenzi wa miundombinu ya madarasa kwenye Shule za Msingi na Sekondari ili waweze kujenga madarasa mengi na kwa gharama nafuu.

Mhandisi Robert Gabriel amebainisha hilo wakati wa ziara yake katika Halmashauri ya Mji wa Geita hivi karibuni ambapo kwa kushirikiana na wananchi wa meneo hayo alichimba misingi ya ujenzi wa madarasa katika Shule za Msingi Mgusu na Uwanja katika kata ya Nyankumbu.

Mkuu wa Mkoa wa Geita amewahamasisha wananchi kutumia teknolojia hiyo kwa sababu kwa gharama ya shilingi milioni 11 tu ujenzi wa darasa moja na la kisasa unakamilika tofauti na matofali ya saruji ambapo darasa moja hujengwa kwa zaidi ya shilingi milioni 20.

Mhandisi Robert Gabriel alitumia fursa ya ziara hiyo  kutoa darasa kwa viongozi wa Kata za Mgusu na Nyankumbu kwa kuwakumbusha viongozi hao kuwa wabunifu,waaminifu, waadilifu, wenye hekima na buasara, wanyenyekevu na wasio na tamaa. Pia kiongozi anatakiwa atambue raslimali zinazomzunguka na kutambua namna zitakavyoinufaisha jamii nzima.

Diwani wa Kata ya Nyankumbu Mhe. Paschal Sukambi amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Geita kwa kuwapatia fedha za awali ambazo wamenunua saruji na matofali na kufanya ujenzi wa shule shikizi ya Uwanja kuanza ambaopo itakapokamilika itasaidia kupunguza msongamano wa wanafunzi katika shule za Nyankumbu na Ukombozi pamoja na kuwanusuru wanafunzi na ajali za barabarani wanapovuka kutoka nyumbani kwenda shule na  wakati wa kurudi.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita Mhandisi Modest Apolinary amewasihi wananchi wa Nyankumbu kubadilisha mitazamo na kushiriana na Serikali katika kuchangia shughuli za maendeleo. “Igeni mfano wa Kata za Shiloleli na Bung’wangoko ambazo ziko pembezoni mwa mji wa Geita lakini wamejitoa kwa hali na mali katika ujenzi wa maboma ya madarasa na baada ya hapo Halmashauri ilitoa fedha za ukamilishaji.” Aliongeza Mhandisi Modest Apolinary.

Matofali fungamano( Interblocking) ni matofali ambayo yanatumika katika ujenzi wa majengo kwa kuyapanga yenyewe pasipo kujengea kwa kutumia mchanga na saruji kama matofali mengine, matofali hayo yanatengenezwa na kikundi cha Nyakatoma Hyrdoform brick making kilichopo Gieta mjini ambao wameajiriwa na Halmashauri ikiwa ni mkakati wa Halmashauri kuwatumia vijana katika shughuli zake za maendeleo.




Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa