• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Shule Ya Nyanza Kujengewa Choo Bora na Cha Kisasa

Posted on: August 21st, 2020

Nyanza Kujengewa Choo Bora na cha Kisasa

Kampuni ya Uchimbaji Madini Ardhini( African Underground Mining Services) ambayo inafanya kazi ndani ya Mgodi wa Dhahabu Geita imetoa ahadi ya kujenga choo bora na cha kisasa kwa ajili ya wanafunzi wa kike wanaosoma katika Shule ya Msingi Nyanza Halmashauri ya Mji wa Geita.

Ahadi hiyo imetolewa na Meneja Mradi wa Kampuni ya AUMS Ndg. Tom (Chris) Sawyer hivi karibuni wakati wa hafla fupi ya  kukabidhi  madarasa matano na ofisi moja ya walimu ambayo yamefanyiwa ukarabati na kampuni yake, hafla iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Nyanza.

Ndg. Sawyer amesema kuwa kampuni yake imeshirikiana na Serikali katika ukarabati wa Shule ya Msingi Nyanza ikiwa ni sehemu ya wajibu wa Kampuni kwa jamii inayowazunguka. AUMS inafurahi kuona vijana ambao ni nguvukazi ya Taifa wanapata elimu kwenye mazingira rafiki ndio maana watahakikisha wanafunzi wa kike ambao wanahitaji kupata choo wanajengewa mapema iwezekanavyo.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ameishukuru kampuni ya AUMS kwa kutambua thamani ya watoto na kutimiza wajibu wao, na ameiomba kampuni hiyo kuichukulia shule ya Msingi Nyanza kama sehemu yao na kuwaomba waisaidie Serikali kukarabati majengo ya madarasa yaliyosalia ambayo hayana muonekano mzuri.

“WanaGeita tuna mila yetu ya kuhakikisha Mkoa wetu unakuwa na maendeleo ya kuigwa hivyo Mkuu wa Wilaya nakuagiza kuyaeleza makampuni mengine yanayofanya kazi ndani ya Mgodi wa Dhahabu wa Geita kushirikiana na Serikali kwa kuchangia utekelezaji wa miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali kama ilivyofanya kampuni ya AUMS.” Aliongeza Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Kijana Ally Salum ambaye ni mwanafunzi wa Darasa la saba katika Shule ya Msingi Nyanza ameishukuru Kampuni ya AUMS kwa kuwathamini na kuwafanya wasome kwenye madarasa ambayo yanalingana na shule za binafsi. Kadhalika kumalizika kwa ukarabati wa  madarasa hayo kumewarahisishia walimu wao kufundisha kwa nafasi kwani hapo awali walikuwa wakibanana sana hali iliyokuwa ikiwajengea hofu ya kutofanya vizuri kitaaluma.

Akitoa neon la shukrani kwa niaba ya uongozi wa shule hiyo, Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Nyanza Bw. Cliford Kassim ametoa shukrani kwa Kampuni ya AUMS, Mkuu wa Mkoa wa Geita, uongozi wa Halmashauri ya Mji Geita na kamati ya ujenzi kwa ushirikiano waliouonesha katika kuhakikisha madarasa yanakarabatiwa na kuleta maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

Ukarabati wa majengo ya madarasa chakavu matano na Ofisi moja ya walimu umetekelezwa kwa ushirikiano wa pande mbili ambapo kamuni ya Afican Underground Services imechangia shilingi milioni 50 za kitanzania na Halmashauri ya mji Geita imetoa zaidi ya Shilingi Milioni 11 mpaka ukamilishaji.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa