• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Shule Maalum Za Wasichana Kuongeza Wanasayansi

Posted on: July 14th, 2023

Shule Maalum Za Wasichana Kuongeza Wanasayansi 

Ujenzi wa Shule maalum za wasichana ambazo zitadahili wanafunzi wa masomo ya sayansi pekee zimebainika kuongeza idadi ya wanafunzi hususan wa kike wa fani mbalimbali za sayansi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Idara ya Elimu Sekondari Halmashauri ya Mji wa Geita Mwalimu Rashid Muhaya alipokuwa akiongea na mwandishi wa Habari hii hivi karibuni Ofisini kwake alipokuwa akitoa ufafanuzi wa mapokezi ya fedha hizo na mikakati ya ujenzi wa shule hiyo ya Kitaifa ambayo itajengwa katika Kata ya Bombambili Geita mjini.

Mwalimu Muhaya ameeleza kuwa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na  Serikali za Mitaa ( TAMISEMI)  kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia mradi wa kuboresha Elimu ya Sekondari( SEQUIP) imetoa fedha kwa Halmashauri ya Mji wa Geita kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya bweni ya wasichana ya kitaifa kwa ajili ya masomo ya sayansi ikiwa na lengo la kuongeza fursa  kwa wanafunzi wa kike kupata nafasi zaidi za kujiunga na masomo ya michepuo ya sayansi.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita Profesa Godius Kahyarara amewaagiza wataalamu wa Halmashauri  kusimamia na kufanya ufuatiliaji wa ujenzi ipasavyo ili kuhakikisha ujenzi unakuwa bora na wenye kuzingatia thamani ya fedha itakayotumika. Pia wanatakiwa kufuata mwongozo wa ujenzi ipasavyo ili ujenzi wa miundombinu iliyopangwa ikamilike kabla au ifikapo mwezi Disemba 2023.

Kulingana na takwimu zilizopo katika Shule zinazopokea wanafunzi wa kike kwa kidato cha tano na sita zina uwezo wa kupokea wanafunzi 316 pekee, ambapo katika kuongeza idadi ya wanafunzi wa kike katika michepuo ya sayansi Halmashauri ya Mji wa Geita imepatiwa Shilingi Bilioni tatu na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kujenga shule maalum ya wasichana ya masomo ya sayansi, ambapo mpaka ukamilishwaji wake itatumia kiasi cha Shilingi Bilioni nne za kitanzania.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa