• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Serikali Yapongezwa Kwa Kukuza Uwekezaji

Posted on: September 28th, 2023

Serikali Yapongezwa Kwa Kukuza Uwekezaji

Mbunge wa Geita Mjini Mheshimiwa Costantine Kanyasu ameipongeza Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kujenga mazingira mazuri na wezeshi kwa wawekezaji hususan wa sekta ya madini ambao umewezesha kuvutia wawekezaji wengi wa madini katika Mkoa wa Geita kwa ujumla.

Pongezi hizo zimetolewa na Mbunge Kanyasu hivi karibuni alipokuwa akizungumza na washiriki wa kongamano la kujadili fursa za kiuchumi na uwekezaji zinazopatikana katika Mkoa wa Geita lililofanyika katika ukumbi wa Mkapa EPZA Bombambili Geita mjini hivi karibuni, ikiwa ni sehemu ya programu ya Maonesho ya sita ya kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea mjini Geita.

Mhe. Kanyasu amesema kuwa uwekezaji mkubwa wa madini ya dhahabu unaofanywa na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya nchi unaendelea kuleta mabadiliko makubwa ya maendeleo na ukuaji wa mji wa Geita kwa kasi kubwa.

“Sisi kama viongozi wa mji huu tumejipanga vyema kuhakikisha uwekezaji katika sekta ya madini ya dhahabu unakuza uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla kwa kuendelea kushirikiana na Serikali katika kutoa fursa kwa wawekezaji kuja kuwekeza katika mkoa wa Geita.” Aliongeza Mhe. Kanyasu.

Mbunge Kanyasu kupitia jukwaa hilo ameiomba Serikali kupitia Wizara ya madini kuendelea kutatua changamoto mbalimbali zilizopo Geita likiwemo suala la vigingi na mipasuko linalotokana na wananchi kutolipwa fidia zao huku akimpongeza Waziri wa Madini wa awali Dkt. Doto Biteko kwa kuacha alama kubwa katika sekta ya madini.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita amesema kuwa wakurugenzi katika mkoa wa Geita wanaendelea kubainisha na kutenga maeneo ya uwekezaji ikiwemo kuweka mazingira rafiki kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi. Pia amewaahidi wachimbaji kutoachwa nyuma na fursa zilizopo katika mji wa Geita kwa sababu kipaumbele ni kwa watu wa Geita kwanza na baada ya hapo ni kwa watu wanaotoka nje ya mkoa.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa