• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Sekta Ya Madini Yazidi Kupaa Kiuchumi

Posted on: October 2nd, 2020

Sekta  Ya Madini Yazidi Kupaa Kiuchumi

Sekta ya Madini chini Tanzania imeendelea kukua zaidi na kuongeza pato laa Serikali katika miaka ya hivi karibuni. Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji Mheshimiwa Angellah Kairuki wakati wa hafla ya ufungaji wa Maonesho ya Tatu ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye sekta ya Madini yaliyofanyika mjini Geita kuanzia Tarehe 17-27/9/2020 katika eneo maalum la uwekezaji kiuchumi  Bombambili.

Mheshimiwa Kairuki amefafanua kuwa Sekta ya Madini imekuwa kwa kiwango kikubwa ambapo mwaka 2015 sekta hiyo ilikuwa ikichangia pato la Taifa kwa asilimia 3.4 lakini kwa sasa mchango wake umepanda hadi kufikia asilimia 5.2, kadhalika ametumia fursa hiyo kuwapongeza wachimbaji wadogo na wafanyabiashara wa madini kwa kulipa kodi kwa hiyari na kufanya kazi zao kwa kufuata sharia, kanuni na taratibu zilizowekwa na Serikali.

Kwa upande wake Waziri wa Madini Mheshimiwa Dotto Biteko amesema kuwa Serikali imeendelea kutekeleza  mipango ya kuwawezesha wachimbaji wadogo ili waweze kufanya shughuli zao kwa tija na kuwaboreshea mazingira yao ya kazi pamoja na kuwatengea maeneo yenye taarifa za kijiolojia ili kuepusha kuchimba kwa kubahatisha.

Mhe. Dotto Biteko pia ametoa wito kwa wachimbaji wadogo na wafanyabiashara wa Madini kuyatumia Maonesho hayo kama chachu ya kuwahimiza kutumia teknolojia nafuu na zenye tija katika shughuli zao.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ameeleza kuwa kwa mwaka 2020 dhahabu iliyopatikana katika Mkoa wa Geita ni zaidi ya tani tano yenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni 576 kutoka kwa wachimbaji wadogo. Haya ni mageuzi makubwa yaliyopatikana ndani ya Mkoa wa Geita katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Tano.

Maonesho ya Tatu ya Kimataifa katika Uwekezaji wa Teknolojia ya Madini yaliyofanyika kwa siku kumi katika Mkoa wa Geita yamehusisha washiriki mbalimbali zikiwemo Wizara mbalimbali, Mashirika ya Umma,Makampuni yanayojishughulisha na uchimbaji wa Madini, Taasisi mbalimbali za Serikali na Sekta binafsi, Umoja wa Wachimbaji wadogo Mkoa wa Geita(GEREMA) Taasisi za kifedha na wajasiriamali wadogo wanaofanya kazi kwa kushirikiana na Shirika la Viwanda vidogo vidogo( SIDO) kanda ya ziwa.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa