• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Plan International Yaunga Mkono Mapambano Dhidi ya Corona

Posted on: April 20th, 2020

Plan International Yaunga Mkono Mapambano Dhidi ya Corona

Shirika la Plan Inernational limeunga mkono juhudi za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika jitihada za kuhakikisha wanapambana kudhibiti maambukizo ya Virusi vya COVID-19.  Shirika hilo limewezesha mafunzo juu ya namna ya kujikinga na Virusi vya COVID-19  kwa watu wenye ulemavu wapatao 100 kutoka Halmashauri mbili za Wilaya ya Geita Tarehe 16-17/4/2020 katika ukumbi wa Chuo cha Afya na Uuguzi Geita mjini.

Akizungumza kwa niaba ya shirika hilo Meneja Mradi Mkoa wa Geita Ndugu Adolf Kaindoa amesema kuwa Shirika la Plan kama wadau wa maendeleo katika Mkoa wa Geita walipata wazo la kuwaseminisha watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali kwa sababu wana haki ya kufahamu namna ya kujikinga na maambukizi ya ugonjwa huo wao binafsi pamoja na familia zao.

Ndg. Kaindoa ameongeza kuwa mafunzo hayo ni sehemu ya kuwajengea uelewa na ufahamu wananchi juu ya mbinu za kukabiliana na janga la Corona, pia njia nyingine zinazoendelea kutumika ni pamoja na vipeperushi, mabango yenye maelezo, matangazo kupitia vyombo vya habari vilivyoko ndani ya Mkoa lengo likiwa ni kuijengea jamii uelewa, utambuzi wa dalili za maambukizi na namna sahih za kujilinda na COVID-19.

“Katika kipindi cha mlipuko wa ugonjwa wa COVID-19 tutaendelea kushirikiana na Serikali kuimarisha ulinzi wa watoto, kupambana na vitendo vya unyanyasaji wa kijnsia, mimba zisizotarajiwa na ndoa za utotoni katika kipindi hiki ambacho wanafunzi wako majumbani muda wote ikiwa ni jitihada ya Serikali kuzuia maambikizi ya ugonjwa wa Corona”. Aliongeza Adolf Kaindoa.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel  amelishukuru Shirika la Plan International kwa kufadhili mafunzo hayo kwa lengo la kuwapa elimu ya COVID-19 watu wenye ulemavu kwa kutambua kuwa virusi hivyo havibagui hali ya mtu. Pia kupitia mafunzo hayo tutaendelea kuzuia  maambukizi mkoani Geita na hatimaye kupunguza au kumaliza kabisa kusambaa kwa virusi hivi nchi nzima.

Mhandisi Robert Gabriel ametumia fursa hiyo kuwasihi wakazi wa Mkoa wa Geita kutowaonea haya wageni wao kutoka Mikoa mingine ambao wana malengo ya kuwatembelea katika kipindi hiki cha mlipuko wa ugonjwa wa Corona wasitishe safari zao mpaka hali itakapokuwa shwari. Kadhalika ana imani kuwa washiriki wa mafunzo hayo wamepata elimu stahiki na uelewa mzuri juu ya virusi  hivyo, njia sahihi za kujikinga, dalili za maambukizi na hatua stahiki za kuchukua ikiwa mtu atapata maambukizi.

Kwa upande wa watu wenye ulemavu, Mwenyekiti wa shirikisho la watu wenye ulemavu Mkoa wa Geita Bw. Robert Kinso ametoa shukrani za dhati kwa shirika la Plan International na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwakumbuka watu wenye ulemavu kwa sababu ni kundi ambalo mara kadhaa husahaulika kushirikishwa katika masuala muhimu yanayoendelea katika jamii. Pia ameomba elimu hiyo iwafikie wenzao walioko katika wilaya nyingine za Mkoa wa Geita licha  ya wao pia kuahidi kufikisha elimu hiyo kwa wenzao ambao wana ulemavu wa kushindwa kutembea wala kutambaa pasipo msaada wa jamaa zao wa karibu.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa