• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Mwenge Wa Uhuru Wazindua Klabu Ya Tehama Nyankumbu Sekondari

Posted on: October 15th, 2021

Mwenge Wa Uhuru Wazindua Klabu ya Tehama Nyankumbu Sekondari

Kiongozi wa Mbio maalum za Mwenge wa Uhuru 2021 Luteni Josephine P. Mwambashi amezindua rasmi klabu ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika shule ya Sekondari ya Wasichana Nyankumbu hivi karibuni wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Wilayani Geita.

Akizindua klabu hiyo ambayo ni mpya Kiongozi wa Mbio maalum za Mwenge wa Uhuru amewaasa wanachama na wanafunzi  wasio wanachama kutumia Tehama kwa manufaa ya kujifunza masuala mbalimbali kwa urahisi zaidi  na sio kufanya utapeli na kuangalia picha zilizo kinyume na maadili ya kitanzania.

“Tehama ni njia mahsusi ambayo imekuwa na mchango mkubwa katika kuleta maendeleo, wanafunzi mmepata fursa ya kujisomea vitabu na masuala mtambuka kupitia njia za kielektroniki. Kadhalika  jamii nzima inakumbushwa kuitumia kwa usahihi na uwajibikaji ili iwasaidie watanzania katika sekta za biashara, elimu, kilimo na uvuvi.” Aliongeza Luteni Josephine Mwambashi.

Akiwa katika shule ya Sekondari ya wasichana Nyankumbu, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru amezindua pia klabu ya wapinga rushwa na kuwakumbusha wanafunzi kuwa rushwa ni adui wa haki na kizuizi kikubwa katika kuleta maendeleo hivyo wanafunzi wana wajibu wa kuhakikisha kila mtanzania anashiriki kupambana na rushwa, wanafunzi wanatakiwa waendelee kutoa elimu katika jamii kwa sababu vijana ndio taifa la leo na nguvu kazi ya taifa pia wategemewa ambao wataongoza nchi miaka ya mbeleni.

Kikundi cha vijana cha Ufunuo ambacho kilipatiwa mkopo na Halmashauri ya Mji wa Geita na kununua magari matatu maarufu kama kirikuu kwa ajili ya biashara ya kusafirishia mizigo wamepongezwa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge kwa kutoona ulemavu kama ugonjwa na kukaa bure majumbani, bali wao wametumia fursa iliyotolewa na Serikali kujikwamua wao binafsi na familia zao.

Mwenge wa Uhuru pia umezindua shamba la miti lenye ukubwa wa hekta 25 lililomea miti 27,700 mali ya Ndugu Paul Kyando. Akizungumza baada ya uzinduzi wa shamba hilo kiongozi wa Mbio maalum za Mwenge wa Uhuru mwaka 2021 amempongeza mkulima huyo kwa kuajiri vijana 40 katika shamba lake na kuongeza kuwa uwepo wa shamba hilo unasaidia uhifadhi wa mazingira na itakapovunwa itasaidia kuongeza mapato ya Halmashauri.

Ukiwa Wilayani Geita Mwenge wa Uhuru 2021 uliobeba ujumbe mkuu usemao ‘ TEHAMA NI MSINGI WA TAIFA ENDELEVU; ITUMIE KWA USAHIHI NA UWAJIBIKAJI’ umekimbia umbali wa kilomita 85.2 na kufungua, kuzindua na kutembelea miradi 11 yenye thamani ya Shilingi Bilioni 11.5, Miradi mingine iliyopitiwa na Mwenge wa Uhuru ni Pamoja na Shule ya Msingi Uwanja, Barabara ya Madini- KKKT, Kikundi cha vijana Safina, Barabara ya Upendo Dispensary- American chips, Hospitali ya Wilaya Katoro, Mradi wa maji Katoro na Klabu ya kupinga matumizi ya dawa za kulevya Shule ya Sekondari Geita.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa