• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

MWAKYEMBE: MNAOTAFUTA FURSA WEKEZENI GEITA

Posted on: August 16th, 2018

WAZIRI wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe,  amewahimiza watafuta fursa za uwekezaji wazingatie kuwekeza kwenye maeneo yenye uhakika wa kupata malighafi na soko, na moja ya eneo hilo ni mkoa wa Geita.

Waziri Mwakyembe aliyasema hayo jana wakati akifungua Jukwaa la Fursa za Biashara Geita lililofanyika jana mjini Geita. Jukwaa hilo lilianza juzi kwa maonesho ya bidhaa  zinazozalishwa hapa Geita.

“Ni vyema wawekezaji wazingatie kwamba viwanda havitafanya vizuri sana kama havitapata malighafi katika eneo husika. Geita ina fursa nzuri ya kuwa na viwanda vinavyotegemea mazao ya migodi, samaki, kilimo na mifugo,” alisema

Alisema Geita pia ina fursa ya soko kutokana na jiografia yake kwa kupakana au kuingiliwa karibu na nchi nyingi zinazounda Jumuiya ya Afrika Mashariki.

“Nimedokezwa hapa kwamba kwa sasa sato wanaovuliwa Geita ni wakubwa na wengi. Katika hali hiyo ni kwa nini Geita isiwe na kiwanda cha kusindika minofu ya samaki?” alihoji.

Aliwaambia washiriki takribani 400 waliohudhuria katika jukwaa hilo kukumbuka kwamba ujio wa wadau mbalimbali wa maendeleo kwenye jukwa hilo vikiwemo vyombo kadhaa vya fedha ni kwa sababu wanajua Geita kuna fursa.

“Ukiona wadau wengi wamekuja hapa Geita basi jua kwamba wameshagundua fursa zilizopo Geita na hivyo wamekuja kujitambulisha na kuwa tayari kutumia fursa inayopatikana Geita,” alisema Waziri Mwakyembe. Alisema Jukwaa hilo lililofanyika jana ni nafasi nzuri kuieleza dunia yale yanayopatikana Geita na pia kuwawezesha wana Geita kujenga uhusiano mpya na wadau mbalimbali.

Dk Mwakyembe alitoa pongezi kwa uongozi wa TSN kwa kutangaza vyema Jukwaa la Biashara na kuwafanya Watanzania na watu wengine katika Afrika Mashariki na dunia kwa ujumla kujua yanayoendelea hapa Geita.

Alisema majukwaa ya biashara yako bega kwa bega na dira ya nchi yetu ya kuipeleka nchi katika uchumi wa kati.

“Lengo kubwa la majukwa haya ni kuamsha ari ya wafanyabiashara na wawekezaji katika kuitikia wito wa Rais John Magufuli ya kufanya nchi yetu kuwa ya uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025,” alisema.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Geita, Robert Gabriel alikaribisha wawekezaji katika mkoa wake akisema wamejipanga kuhakikisha kwamba mwekezaji yeyote anayekuja Geita hazungushwi wala kuomba rushwa.

“Geita ni mkoa rafiki kwa mwekezaji. Hapa tumekataa urasimu, na hakuna kuzungushwa. Anayetaka kuwekeza Geita tunamshughulikia kwa siku chache tu. Tuko wakali sana kwa mwekezaji anayezungushwa hata siku moja tu.

“Urasimu, kuzingushwa zungushwa na kuombana rushwa hapa Geita tunaita zilipendwa… Kwenye rushwa hata maua yanakauka, rushwa inazuia mkoa kunyanyuka,” alisema.

Mkuu wa mkoa alisema kutokana na jiografia yake Geita ni sehemu nzuri ya kuwekeza kuliko maeneo mengi ya Afrika Mashariki

Aliufafanisha mkoa wake na nchi ya ahadi akisema karibu kila kitu kinachoelezwa katika vitabu kuhusu nchi ya ahadi vinapatikana Geita.

Aliongeza: “Geita Mungu alishaifanya kuwa tajiri, tunachoomba sasa ni  Mungu atupe jicho la kuona raslimali tuliyo nayo na kuisimamia vyema,” alisema





Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa