• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Mradi wa SEQUIP Kuwakomboa Wanafunzi Zaidi ya 180 Geita

Posted on: August 9th, 2022

MRADI WA SEQUIP KUWAKOMBOA WANAFUNZI ZAIDI YA 180 GEITA

“Tunasoma kwa taabu, mvua hutunyeshea, jua kutuwakia, tunakimbizwa na wanyama wakali kama fisi, dada zetu wanakumbana na vishawishi kutoka kwa vijana wawapo njiani kuelekea nyumbani na kikubwa Zaidi tunafika majumbani tukiwa tumechoka sana na kushindwa kujisomea muda wa ziada.” Kauli ya Joseph Mwebeya mmoja wa wanafunzi wanaosoma katika Shule ya Sekondari Bulela akitokea kata jirani ya Shiloleli.

Mayala Samike, mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari Bulela ni miongoni mwa wanafunzi wanaotembea umbali mrefu kufika shuleni, ambaye amesema kushinda na njaa Pamoja na kukosa vipindi vya kwanza darasani imekuwa sehemu ya Maisha yao hali inayopelekea kuzorota kwa uwezo wake kitaaluma kwani wakirejea nyumbani baada ya masomo wanakuwa na uchovu ambao huwalazimu kulala na kushindwa kupata muda wa kujisomea.

Kukamilika kwa ujenzi wa Shule mpya ya kwanza ya Sekondari katika kata ya Shiloleli Halmashauri ya Mji wa Geita ambayo iko katika hatua za ukamilishwaji kupitia mradi wa SEQUIP kutoka Serikali kuu kutawatatulia changamoto ya kutembea umbali wa kilomita 16 kwa safari moja wanafunzi wa kata hiyo ambao kwa sasa wanakwenda kupata masomo yao katika Shule ya Sekondari Bulela iliyoko kata ya Jirani.

Akizungumza na mwandishi wa Habari hii hivi karibuni, Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari Bulela Mwalimu Pelicia Ponsian ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuwakumbuka wanafunzi wa Shiloleli na kuona umuhimu wa kupata shule katika mazingira yao.

Mwalimu Ponsian amesema kuwa uwepo wa shule hiyo mpya utawasaidia wanafunzi wanaotaraji kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023 pamoja na wanafunzi 183 wanaosoma katika shule yake wanaotoka kata ya Shiloleli ambapo wanatembea umbali mrefu na wakati mwingine hususan kipindi cha masika wanakwama kufika shuleni au kufika shule kwa kuchelewa na kukuta masomo yameshaanza kufundishwa.

Mwalimu Ponsian ameongeza kuwa  changamoto nyingine ni matokeo ya wanafunzi hao yamekuwa si ya kuridhisha kwa sababu uelewa wao darasani hupungua kutokana na uchovu wa safari ya kutoka nyumbani hadi shule, kushinda njaa, utoro wa rejareja ambao husababishwa na sababu zilizo nje ya uwezo wa wanafunzi kama uwepo wa wanyama wakali na vibaka  kwenye mapori wakati wa kwenda shuleni.

Kwa upande wa Diwani wa Kata ya Shiloleli Mhe. Boniphace Kaswahili Fulano amesema yeye ameunga mkono juhudi za Serikali kwa kutoa bure eneo lake lenye Zaidi ya ekari tisa ili shule ya Sekondari ya kwanza iweze kujengwa na kuwanufaisha Watoto wa kata hiyo. Pia ametoa wito kwa wazazi kuwahamasisha Watoto kupenda shule kwani elimu ndiyo ufunguo wa Maisha.

Afisa Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Mji Geita Ndugu Rashid Muhaya amesema kuwa kutokana na changamoto ya mdondoko wa wanafunzi inayosababishwa na umbali mrefu katika bajeti ya mwaka 2022/2023 Halmashauri imelenga kujenga shule mpya nne katika kata mbalimbali ambazo zitagharimu Shilingi Bilioni 1.07

Shule mpya ya Sekondari katika Kata ya Shiloleli ni miongoni mwa shule mpya 11 za Sekondari zilizojengwa katika Halmashauri ya Mji Geita kwa lengo la kupunguza msongamano wa wanafunzi darasani na kuwaondolea adha ya kutembea umbali mrefu kufika shule kwa baadhi ya wanafunzi wanaotumia muda mwingi kutembea mpaka shuleni kwa ajili ya masomo.

“Ndani ya miaka mitatu iliyopita Halmashauri ya Mji wa Geita tumefanikiwa kujenga shule 11 za sekondari ambazo kwa kiasi zimesaidia kupunguza changamoto ya wanafunzi ambao hutembea umbali mrefu na kuondoa msongamano wa wanafunzi darasani.” Aliongeza Ndg. Muhaya.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia mradi wa kuboresha elimu wa SEQUIP imetoa kiasi cha shilingi milioni 470 kwa ajili ya ujenzi wa shule hiyo ili kuwanusuru wanafunzi wanaotembea umbali wa kilomita 18 hadi 32 kwenda shule na kurudi nyumbani. Mpaka sasa Halmashauri ya Mji Geita ina shule za 19 za sekondari ambapo wanafunzi wa shule sita wanalazimika kutembea umbali mrefu kwenda na kukudi shule.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa