• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Mradi wa BOOST Kupunguza Msongamano wa Wanafunzi

Posted on: April 19th, 2023

Mradi Wa BOOST Kupunguza Msongamano wa Wanafunzi

Halmashauri ya Mji wa Geita inatarajia kujenga shule mbili mpya za msingi kupitia mradi wa kuimarisha na kuboresha elimu ya awali na msingi (BOOST) kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Akizungumza wakati wa uwasilishaji wa taarifa ya maandalizi ya utekelezaji wa mradi huo, Kaimu mratibu wa BOOST Bi. Rahel Mwera ameeleza kuwa Halmashauri ya Mji Geita inatarajia kupokea Shilingi 1,080,600,000/= ambazo zitatumika katika ujenzi wa shule mbili mpya za msingi katika kata ya Buhalahala.

Bi. Rahel Mwera ameeleza kuwa shule hizo mpya zitajengwa katika mtaa wa Mwatulole ambako baada ya uchambuzi wa tathimini ya mahitaji na hali ya miundombinu ya shule za msingi katika Halmashauri zote 184 nchini Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za mitaa ilibaini kuelemewa kwa shule za msingi Mwatulole na Ngunzombili kutokana na idadi kubwa ya wanafunzi isiyowiana na idadi ya madarasa yaliyopo kwa sasa.

Kupitia mradi wa BOOST Halmashauri ya Mji Geita inatarajia kupokea Shilingi 1,653,300,000/= itajenga vyumba 18 vya madarasa katika shule tofauti, madarasa mawili ya mfano kwa elimu ya awali, chumba kimoja cha darasa la elimu maalum na matundu 13 ya vyoo.

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilitoa maagizo kwa Halmashauri zote nchini kuhakikisha fedha zinazotolewa katika utekelezaji wa miradi hiyo zinakamilisha ujenzi kama ilivyopangwa ili kuepusha miradi mingi kutokamilika huku fedha zikiwa zimekwisha. Pia thamani ya fedha itakayotolewa iendane na majengo yatakayojengwa ili kufikia matokeo yaliyokubalika.

Mradi wa BOOST utatekelezwa katika kipindi cha miaka mitano kuanzia 2021/2022 hadi 2025/2026 ambapo utatekelezwa kwa awamu tofauti. Mkoa wa Geita utapokea Shilingi 9,781,100,000 kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya 11, vyumba vya madarasa 143 ya Shule za Msingi, vyumba vya madarasa ya mfano ya Elimu ya Awali 12, chumba kimoja cha darasa kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalum na matundu 94 ya vyoo.


Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WANAFUNZI WA KOZI YA AWALI YA JESHI LA AKIBA WAPATIWA ELIMU YA HABARI

    July 04, 2025
  • WATUMISHI WAKUMBUSHWA KUFANYA KAZI KWA UMOJA

    June 30, 2025
  • BONAZA LA WATUMISHI WA HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA NA HALMASHAURI YA WILAYA YA KWIMBA

    June 28, 2025
  • WANANCHI WA MANISPAA YA GEITA WAKUMBUSHWA KUENDELEA KUFANYA USAFI

    June 28, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa