• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

MPANGO WA TPRP KUNUFAISHA WANANCHI GEITA

Posted on: August 22nd, 2022

MPANGO WA TPRP KUNUFAISHA WANANCHI GEITA

Kukamilika kwa ujenzi wa miundombinu ya elimu ambayo iko katika hatua ya ukamilishwaji kupitia Mpango wa kupunguza Umaskini Tanzania (TPRP) inayotekelezwa kwa ushirikiano wa Halmashauri ya Mji wa Geita na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Nchini( TASAF) kutawanufaisha wananchi waishio katika mitaa ya Nyanza, Bombambili, Kivukoni, Mwatulole na Shinde.

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Mji Geita Ndugu Upendo Kilonge wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo iliyofanywa na wajumbe wa Timu ya Menejimenti ya Halmashauri ya Mji wa Geita hivi karibuni.

Ndg. Upendo Kilonge amefafanua kuwa mwezi machi 2022 Halmashauri yake ilipokea Shilingi 411,307,414.58 kutoka Serikali kuu kwa ajili ya utekelezaji wa ujenzi wa miundombinu ya shule na wanajamii walioko kwenye maeneo ya utekelezaji wa miradi wamechangia kiasi cha shilingi 25,159,519 kwa lengo la kuhakikisha miradi hiyo inakamilika kwa wakati na kuwasaidia wanafunzi, walimu na jamii kwa ujumla.

“Miradi inayotekelezwa kupitia mpango wa TPRP ni Ujenzi wa jengo la utawala Shule ya Sekondari Nyanza, Ujenzi wa bweni la wavulana katika shule ya Sekondari Mwatulole, Ujenzi wa jengo la utawala Shule ya Sekondari Bombambili, Ujenzi wa madarasa mawili, ofisi moja ya walimu na choo cha matundu sita katika Shule ya msingi Kivukoni ambapo mpaka sasa miradi yote imetumia kiasi cha shilingi 394,024,011.10”. Aliongeza Ndg. Upendo Kilonge.

Ndugu Kilonge ameeleza kuwa ujenzi wa miradi hiyo inatekelezwa kwa kutumia mafundi wa jamii( local fundi) kwa kushirikiana na wananchi wa ngazi zote chini ya usimamizi wa kamati maalum( CMC) ngazi ya jamii ambao wamepatiwa mafunzo, wawezeshaji kutoka Halmashauri ya Mji Geita na timu ya wataalam kutoka TASAF.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwatulole Bi.Roseline Mariki amesema kuwa kukamilika kwa ujenzi wa bweni la wavulana katika shule yake kutawawezesha wanafunzi 80 wa kidato cha tano na sita kutoka katika mikoa mbalimbali kupata fursa ya kuishi bwenini na kupata muda mwingi wa kujisomea.

Mratibu wa TASAF Halmashauri ya Mji Geita amewasihi wananchi kujitoa kwa muda muafaka katika kushiriki kikamilifu katika kazi zote zinazowahusu ili kuweza kumaliza kazi kwa wakati, kadhalika kamati zinazohusika na usimamizi, manunuzi na mapokezi zishiriki kikamilifu katika kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa mwongozo wa usimamizi miradi ili kuwezesha miradi hiyo kukamilika kwa wakati na kuwanufaisha wananchi.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa