• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Mpango Kabambe 2017-2037 Kubadili Mandhari ya Mji wa Geita

Posted on: September 21st, 2021

Mpango Kabambe 2017-2037 kubadili Mandhari ya Mji Geita

Kuzinduliwa kwa Mpango Kabambe wa Mji wa Geita(Geita Town Master Plan) kutawezesha kupanga matumizi ya ardhi kwa ujumla na kukuza fursa za uwekezaji, biashara ,uchumi, utawala, maendeleo ya jamii na kulinda mazingira kwa kipindi cha miaka 20.

Hayo yamebainishwa na Naibu Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya makazi Mheshimiwa Angelina Mabula alipokuwa akiongea na wadau mbalimbali wa maendeleo mjini Geita hivi karibuni wakati wa hafla ya uzinduzi rasmi wa mpango kabambe katika ukumbi wa Gedeco Geita mjini.

Mhe. Angelina Mabula ametoa pongezi za dhati kwa uongozi wa Halmashauri ya Mji Geita kwa uandaaji wa mpango kabambe ambapo amefurahishwa kuona namna kila kiongozi hususan wa siasa wanauelewa vyema mpango wao utakaowawezesha kuuendeleza mji na kudhibiti matumizi ya ardhi yasiyofaa.

Naibu Waziri wa Ardhi alitumia fursa hiyo kumtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Geita kuweka wasimamizi watakaofanya kazi ya kupitia mara kwa mara kusimamia udhibiti wa ujenzi holela na uvamizi wa maeneo ambayo yameainishwa kwenye mpango kabambe. Kadhalika ametoa rai kwa watumishi wa idara ya ardhi kuhakikisha wanautendea haki mpango kabambe  kwa kutopokea maombi ya kubadili mpango wa matumizi ya ardhi usio na tija kwa matashi ya mtu binafsi au kundi la watu Fulani.

Kwa upande wake Mbunge wa Geita mjini Mheshimiwa Costantine Kanyasu amesema kuwa tukio la uzinduzi wa mpango kabambe ni njia ya kuelekea kwenye ndoto ya kuwa manispaa naimani yake juu ya wananchi wa Geita ni kuwa watauishi mpango kabambe huo kwa kutokujenga katika maeneo ambayo yameshaainishwa kwa ajili ya miradi ya huduma za kijamii kama barabara za juu na mengineyo.

Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji wa Geita Mheshimiwa Joseph Lugaila ametoa rai kwa wadau wote wa maendeleo mjini Geita kushirikiana kikamilifu na uongozi wa Halmashauri ya Mji wa Geita katika kuhakikisha lengo la kuupanga mji wa Geita katika viwango vinavyotakiwa tofauti na hali ilivyo kwa sasa linafanikishwa kwa asilimia mia moja na zaidi.

Mpango kabambe uliozinduliwa utakuwa na faida mbalimbali ambazo ni  kuondoa migogoro ya ardhi inayotokana na mwingiliano wa kimatumizi, kutoa fursa za kiuwekezaji kwa viwanda na biashara, kuwa na mji uliopangwa wenye makazi bora, kuhifadhi na kulinda mazingira na kutoa fursa za ujenzi wa miundombinu na huduma za kijamii.



Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA MANISPAA YA GEITA June 03, 2025
  • TANGAZO KUHUSU FURSA ZA MIKOPO YA ASILIMIA 10 May 27, 2025
  • Zaidi

Habari Mpya

  • MKUTANO MAALUMU WA BARAZA WA KUJADILI MAJIBU YA HOJA NA MAPENDEKEZO YA MDHIBITI NA MKAGUZI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    June 11, 2025
  • BILIONI 19.1 KUTEKELEZA UJENZI KITUO KIKUU CHA MABASI MANISPAA YA GEITA

    June 06, 2025
  • WATUMISHI GEITA MANISPAA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA KANUNI ZA UTUMISHI WA UMMA

    June 05, 2025
  • WATUMISHI WA MANISPAA YA GEITA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MITANDAO YA KIJAMII YENYE TAARIFA ZA UPOTOSHAJI

    June 04, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa