Wananchi wa Mwatulole Manispaa ya Geita wamejitokeza kushiriki zaoezi la kufanya usafi katika maeneo mbalimbali ya Halmashauri ya Manispaa ya Geita ikiwa ni jumamosi ya Mwisho wa mwezi huku Mkuu wa wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba, Katibu tawala Wilaya ya Geita Bi. Lucy Beda na Mkurugenzi wa Manispaa ya Geita Ndugu. Yefred Myenzi wakiongoza zoezi hilo
Shughuli hii ya Usafi ni muendezo wa kampeni Ya HYAGULAGA GEITA (SAFISHA GEITA) iliyo zinduliwa na Mhe Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba Tarehe 26 Aprili, 2025 ikiamasisha watu kufanya usafi na kuisafisha Geita kuwa safi na yenyekupendeza
Nae Mkurugenzi wa manispaa ya Geita Ndugu. Myenzi ameendelea kuwasisitiza wananchi kuendelea kufanya usafi kila wakati katika maeneo yao nasio kungoja siku ya Jumamosi pekee ameyasema hayo huku akisisitiza wananchi kuendana na hadhi ya manispaa kwa kuisafisha Geita
Huku Wananchi wa Mwatulole wamesema wanaunga mkono na kumpongeza Mkuu wa Wilaya kwa kampeni hii inayohimiza usafi hakika amezindua vitu vingi ambavyo wanageita tunatakiwa kutoviacha vipite
Naye Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba amewashukuru wote kwa kujitokeze kuendelea na zoezi la usafi
"Nawashukuru kwa kujitokeza kwa wingi na nawaahidi kuhakikisha na kushirikiana nanyi katika kila hatua ili kuuweka mji wetu uwe safi hii itatuepusha na magonjwa ya mlipuko pia tutachukua hatua za kisheria kuwawajibisha wote wanao puuzia zoezi hili" amesema Mhe. Komba.
TUFUATILIE KATIKA MITANDAO YETU YA KIJAMII
Instagram
Geita Tanzania
Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita
Namba ya Simu: 0282520437
Mobile:
Barua pepe: td@geitatc.go.tz
Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa