• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

MILIONI 605 KUTOKA GEITA MJI ZANUFAISHA VIKUNDI 67

Posted on: July 19th, 2022

MILIONI 605 KUTOKA GEITA MJI ZANUFAISHA VIKUNDI

Jumla ya vikundi 67 vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kutoka katika kata mbalimbali za Halmashauri ya Mji wa Geita vimepatiwa mkopo wa Shilingi milioni 605 kwa ajili ya kuviwezesha kutekeleza shughuli mbalimbali za kiuchumi ambapo shilingi 449,000,000 zinatokana na asilimia 10% ya makusanyo ya ndani ya halmashauri na Shilingi 156,000,000/=ni marejesho ya mikopo.

Akitoa mchanganuo wa Shilingi 372,118,000 zilizotolewa kwa vikundi 20 vya vijana, Shilingi 219,882,000 vikundi 45 vya wanawake na Shilingi 13,000,000 vikundi 2 vya watu wenye ulemavu wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika tarehe 18/7/2022 Geita mjini, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Geita Bi. Zahara Michuzi amesema kuwa katika fedha iliyotolewa shilingi 192,800,000/= zimetumika kununua bajaji 21 na pikipiki moja ambazo zimegawiwa kwa vijana wa umoja wa waendesha bajaji mkoa wa Geita.

Bi. Zahara Michuzi ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuendeleza progamu hii ya uwezeshaji wa makundi haya maalum kwani imesaidia kupunguza kero nyingi zilizokuwa zinawakabili wajasiriamali wengi kama ukosefu wa mitaji, wanawake kuondokana na utegemezi kutoka kwa waume zao hali iliyosababisha kuongezeka upendo katika familia na kuongezeka kwa uchumi binafsi wa wanufaika na jamii kwa ujumla.

Akikabidhi hundi na bajaji hizo mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Geita Ndg. Janeth Mobe ameipongeza Halmashauri ya Mji kwa kuendelea kutoa mikopo isiyokuwa na riba kwa makundi maalum na kuwataka wanavikundi kufanya shughuli za uzalishaji mali na kutochukulia fedha hizo kama hisani au sadaka bali wanapaswa kuzirejesha kwa wakati kwa mujibu wa sheria.

“Pamoja na mafanikio mengi mnayoyapata nitumie nafasi hii kuwasihi kuzitunza bajaji na pikipiki mlizokabidhiwa leo ili ziweze kudumu na pia madereva zingatieni sheria za barabarani kwa kuendesha vyombo vyenu kistarabu, kutoruhusu vyombo vyenu vya usafirishaji kutumika katika matukio ya kihalifu kama wizi, ujambazi, magendo nk. Mkionyesha weledi katika shughuli zenu mtakuwa mnaunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vitendo.

Akizungumza kwa niaba ya wanavikundi walionufaika na mkopo huo, Bi. Riziki Ramadhani ambaye ni dreva wa kike pekee wa bajaji  ameipongeza serikali ya awamu ya sita chini ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan na halmashauri ya Mji wa Geita kwa kuendelea kuthamini mahitaji ya makundi maalum jitihada zao za kujikwamua kiuchumi kwa kuwapatia mikopo isiyo na riba . Pia amewasihi wenzake hususan wanawake kufanya kazi zote halali pasipo kuogopa kuchekwa au kubezwa na mtu yeyote.

Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri ya Mji Geita ilitenga Shilingi 909,574,000 kutoka kwenye mapato ya ndani ambazo fedha hizo zimekopeshwa kwa vikundi 115 vya wajasiriamali na katika mwaka huo wa fedha kiasi cha shilingi 658,816,000 kimerejeshwa kutoka kwenye vikundi vya vijana, wanawake na watu wenye ulemavu.


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • SERIKALI YAONGEZA FEDHA ZA ELIMU BURE MANISPAA YA GEITA

    May 11, 2025
  • WASIOFANYA USAFI KATIKA MAENEO YAO KUCHUKULIWA HATUA - DC KOMBA

    May 10, 2025
  • MAFUNZO KWA VIKUNDI VINAVYOTARAJIWA KUPEWA MIKOPO YA ASILIMIA KUMI

    May 09, 2025
  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa