• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Mgusu Wajivunia Mema ya Serikali ya Awamu ya Tano

Posted on: April 3rd, 2020

Mgusu Wajivunia Mema Ya Serikali ya Awamu ya Tano

Maendeleo katika sekta za elimu, afya , utawala bora na nishati ya umeme wa uhakika yanayopatikana katika Kata ya Mgusu iliyoko katika Halmashauri ya Mji wa Geita ambapo mafanikio hayo yameonekana katika kipindi cha uongozi wa awamu ya tano ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yamewawezesha wananchi wa Kata ya Mgusu na mitaa yake kujivunia mema ya nchi yao.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni alipotembelewa katika kata yake, Diwani wa Kata ya Mgusu Mheshimiwa Pastory Ruhusa ameishukuru Serikali ya awamu ya tano chini ya uongozi wa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na watendaji walio chini yake hususan wa Mkoa na Wilaya ya Geita kwa kazi kubwa waliyoifanya katika kuhakikisha Kata ya Mgusu inapata huduma za muhimu za kijamii.

Mhe. Ruhusa amesema kuwa kwa sasa Kata yake imefanikiwa kujenga shule mbili za Sekondari ambazo ni Shule ya Sekondari Mgusu na Shule ya Sekondari Nyakabale ambazo shule zote zilifunguliwa mapema mwaka 2019, Shule ya msingi Manga iliyoko katika mtaa wa Manga, Pia ujenzi wa Shule mpya ya Msingi Machinjioni, ujenzi wa Zahanati ya Mgusu, Ujenzi wa Maabara ya masomo ya sayansi, madarasa mawili na jengo la utawala Shule ya Sekondari Mgusu bado unaendelea.

“Haikuwa jambo rahisi kujenga shule mbili za Sekondari kwa wakati mmoja katika kata yangu, lakini napenda kuwapongeza na kuwashukuru kwa dhati wananchi wangu kwa kujitoa kwa moyo kushirikiana na Halmashauri ya mji wa Geita  katika shughuli za ujenzi wa shule hizi baada ya kutambua namna wanafunzi hususani wa kike wanavyopata shida kutembea umbali mrefu wa zaidi ya kilomita kumi kwenda shule ya Sekondari Shantamine iliyoko katika kata ya jirani ya Mtakuja.” Aliongeza Mhe. Ruhusa

Akiongea kwa niaba ya wananchi wa Kata ya Mgusu Bi. Ziara Peter ambaye ni mkazi wa mtaa wa Mgusu ametoa shukrani za dhati kwa Diwani wa kata yao na Halmashauri ya Mji wa Geita kwa kuwawezesha wananchi wa kata hiyo kupata umeme wa uhakika tofauti na awali walipokuwa wanaishi gizani. Pia wameishukuru Serikali kwa kuwajengea zahanati ambayo baadaya kukamilika itaondoa adha ya kina mama wajawazito kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya kujifungua.

Kata ya Mgusu ni mojawapo ya kata changa ndani ya Halmashauri ya Mji wa Geita, ambapo sehemu kubwa ya wakazi wake hujishughulisha na uchimbaji mdogo wa madini ya Dhahabu,  ilianzishwa  rasmi mwaka 2015 ikiwa na mitaa minne ambayo ni Nyakabale, Manga, Machinjioni na Mgusu. Uongozi wa kata ulipoanza kazi walikuwa na shule mbili za msingi na Zahanati ya Nyakabale pekee, wananchi wa kata hiyo hawakuwa na huduma ya nishati ya umeme wala maji.



Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa