• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Geita Town Council
Geita Town Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Mji wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara
      • Rasilimali Watu na Utawala
      • Mipango na Uratibu
      • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Kilimo, Mifugo na Uvuvi
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Miundombinu, Maendeleo vijijini na Mjini
      • Usimamizi taka na Usafi wa Mazingira
    • Vitengo
      • Michezo, Utamaduni na Sanaa
      • Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi
      • Maliasili na Uhifadhi Mazingira
      • Sheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Usimamizi wa Manunuzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Kitalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uchimbaji Madini
    • Sekta ya Viwanda
  • Huduma Zetu
    • Afya, Ustawi wa jamii na Huduma ya Lishe
    • Elimu
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha na Uongozi
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Elimu na Afya
      • Kamati ya Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Ratiba ya Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
    • Huduma kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu ya Maombi
    • Miongozo
    • Jarida la Halmashauri
    • Mkakati wa kuziwezesha
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya picha
  • Maeneo ya Uwekezaji

Mbio za Mwenge wa Uhuru 2018

Posted on: April 3rd, 2018

Wananchi Wahimizwa Kuwekeza Katika Elimu

Wakazi katika Halmashauri ya Mji Geita wamehimizwa kuhakikisha kuwa wanatumia nguvu zao na raslimali walizonazo kuwekeza katika sekta ya Elimu ili kupambana na adui ujinga na kujenga Taifa litakalozalisha wataalamu katika fani mbalimbali ambao watailetea nchi ya Tanzania maendeleo makubwa.

Rai hiyo imetolewa na Mkimbiza Mwenge wa Uhuru kitaifa mwaka 2018 Ndugu, Charles Francis Kabeho alipokuwa akizindua rasmi madarasa mawili, bwalo la chakula na bweni la wanafunzi katika Shule ya Sekondari Kasamwa wakati wa Mbio za Mwenge wa Uhuru katika Halmashauri ya Mji Geita tarehe 01/04/2018.

Mkimbiza Mwenge wa Uhuru 2018 amewasihi wananchi kuwekeza katika elimu kwa kushiriki kuchangia ujenzi wa  madarasa, mabweni, utengenezaji wa madawati na kujenga vyuo vya ufundi na ufundi stadi ili kuwapa nafasi wanafunzi wanaomaliza kidato cha nne na kukosa nafasi ya kuendelea na kidato cha tano wapate fursa ya kupata elimu ya ufundi.

Ndg. Kabeho aliwapongeza wananchi wa Kata ya Kasamwa na vitongoji vyake kwa kujitoa kikamilifu katika kuchangia fedha na nguvu kazi wakati wa zoezi la ujenzi wa miundombinu hiyo. Aliongeza kuwa wananchi hao wameonyesha namna walivyotambua umuhimu wa elimu katika eneo lao.

Mkibiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2018 amewaasa wazazi na walezi kuhakikisha wanatimiza wajibu wao katika kuwanunulia watoto wao mahitaji muhimu yanayohitajika shule kama sare za shule, madaftari ili kutoruhusu nafasi ya watoto wao kushindwa kuhudhuria masomo kwa kukosa mahitaji ya msingi.

 “Wazazi jitahidini kuwahimiza watoto na vijana wenu kupenda masomo ya sayansi na hisabati ili kupata watu watakaotumika katika uzalishaji wa viwanda mbalimbali vinavyoanzishwa nchini na kupata wataalam wa masomo ya sayansi.” Aliongeza Ndg.  Charles Kabeho.

Ndg. Charles Kabeho alitumia fursa hiyo kuwaagiza wazazi na walezi wote kufuatilia mahudhurio ya wanafunzi shuleni ili kupunguza tatizo la utoro shuleni. Pia aliziagiza idara za Elimu Msingi na Sekondari kufuatilia na kuchukua hatua madhubuti katika kuondokana na tatizo la utoro shuleni, ambapo Mkoa wa Geita ni wa pili kwa tatizo la utoro shuleni kwa asilimia 8.1

Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Sekondari Kasamwa Bi. Agness D. Busanji amepokea agizo hilo na kuahidi kufuatilia kikamilifu mahudhurio ya wanafunzi katika shule yake na kubaini changamoto mablimbali zinazopelekea wanafunzi hao hususani wa kike kutoroka shule, ili wazitatue kwa kushirikiana na Halmashauri ya Mji.

Miundombinu ya madarasa, bwalo la chakula na bweni la wasichana katika Shule ya Sekondari Kasamwa limegharimu kiasi cha Shilingi 444,680,300.00 chanzo cha fedha hizo ni mapato ya ndani ya Halmashauri na mchango wa wananchi. Mradi huo ni moja ya mradi kati ya miradi tisa iliyowekewa mawe ya msingi, kuzinduliwa, kufunguliwa na kutembelewa na Mwenge wa Uhuru 2018 katikaHalmashauri ya Mji Geita, ambapo kwa ujumla wake imegharimu Shilingi 3,374,178,963.00.

 Kauli Mbiu ya Mwenge wa Uhuru 2018 ni “Elimu ni Ufunguo wa Maisha Wekeza sasa kwa Maendeleo ya Taifa letu”.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAHILI WA MAOHOJIANO (ORAL INTERVIEW) KADA YA MWANDISHI MWENDESHA OFISI DARAJA LA II September 27, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI WA MAHOJIANO MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU II September 29, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI July 05, 2024
  • TANGAZO LA KUITWA KATIKA USAHILI September 21, 2024
  • Zaidi

Habari Mpya

  • BURIANI MHE DAVID CLEOPA MSUYA

    May 07, 2025
  • TWCC MKOA WA GEITA WAMEMKABIDHI HATI YA SHUKRANI MKURUGENZI MYENZI

    May 07, 2025
  • ZIARA YA MKUU WA WILAYA YA GEITA MHE. HASHIM A KOMBA KUTEMBELEA NJIA NA MIRADI ITAKAYOPITIWA NA MWENGE WA UHURU 2025

    May 06, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA UONGOZI YAMPONGEZA MKURUGENZI MYENZI

    May 05, 2025
  • Zaidi

Video

WATENDAJI WA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WATAKIWA KUTOJIHUSISHA NA ITIKADI ZA KISIASA
More Videos

Kurasa za Karibu

  • Mfumo wa Watumishi kujihudumia
  • Applications Forms
  • Acts
  • Taarifa za Huduma za Afya
  • Mfumo wa Kupata Leseni za Biashara ( Mfumo wa Tausi)
  • Barua pepe za watumishi
  • Wasiliana nasi
  • Malalamiko
  • Taarifa za Mapato

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti Rasmi ya Rais
  • Tovuti ya Utumishi
  • Tovuti ya OR-TAMISEMI
  • TUWE MFANO KWA TAIFA' Yefred Myenzi
  • Ofisi ya Takwimu ya Taifa
  • Tovuti Kuu ya Serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    Geita Tanzania

    Sanduku la Posta: P.o Box 384 Geita

    Namba ya Simu: 0282520437

    Mobile:

    Barua pepe: td@geitatc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

Visitors Counter

Counter Widgets

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hatimiliki 2017 Halmashauri ya Mji Geita . Haki zote zimehifadhiwa